< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
你們叫我的心悲傷,說話苦惱我,要到何時﹖
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
你們侮辱我,已有十次之多,苛待我卻不知羞愧。
4 Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
我若實在錯了,錯自由我承當。
5 Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
如果你們真要對我自誇,證明我的醜惡,
6 basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
你們應當知道:是天主虐待了我,是他用自己的羅網圍困了我。
7 “Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
我若高呼說:「殘暴,」但得不到答覆;我大聲呼冤,卻沒有正義。
8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
他攔住我的去路,使我不得過去,使黑暗籠罩著我的去路。
9 Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
他奪去了我的光榮,摘下了我頭上的冠冕;
10 Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
他四面打擊我,使我逝去;拔除我的希望,猶如拔樹。
11 Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
他對我怒火如焚,拿我當作他的仇敵。
12 Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
他的軍隊一齊開來,修好道路攻擊我,圍著我的帳幕紮營。
13 “Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
他使我的弟兄離棄我,使我的知己疏遠我。
14 Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
鄰人和相識者都不見了,寄居我家的人都忘了我。
15 Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
我的婢女拿我當作外人,視我如一陌生人。
16 Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
我呼喚僕人,他不回答;我必須親口央求他。
17 Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
我的氣味使妻子憎厭,我的同胞視我作臭物。
18 Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
連孩子們也輕慢我,我一起來,他們就凌辱我。
19 Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
我的知交密友都憎惡我,我所愛的人也對我變了臉。
20 Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
我的骨頭緊貼著皮,我很徼幸還保留牙床。
21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
我的朋友,你們可憐可憐我罷! 因為天主的手打傷了我。
22 Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
你們為何如同天主一樣逼迫我,吃了我的肉還不知足呢﹖
23 “Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,
惟願我的話都記錄下來,都刻在銅板上;
24 kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, au kuyachonga juu ya mwamba milele!
用鐵鑿刻在鉛版上,永遠鑿在磐石上。
25 Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai, naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.
我確實知道為我伸冤者還活著,我的辯護人要在地上起立。
26 Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;
我的皮膚雖由我身上脫落,但我仍要看見天主;
27 mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: mimi, wala si mwingine. Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!
要看見他站在我這一方,我親眼要看見他,並非外人;我的五內因熱望而耗盡。
28 “Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’
如果你們說:「我們怎能難為他﹖怎能在他身上尋到這事的根由﹖」
29 ninyi wenyewe uogopeni upanga, kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”
你們應當害怕刀劍,因為報復罪惡者是刀劍;如此你們知道終有一個審判者。

< Ayubu 19 >