< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Entonces Bildad el suhita respondió y dijo:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
¿Cuánto tiempo pasará antes de que hayas terminado de hablar? muestren entendimiento, y luego diremos lo que está en nuestras mentes.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
¿Por qué parecemos bestias y estúpidos ante tus ojos?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Tu crees que en tu enojo, que te estás desgarrando con rabia, ¿la tierra será desierta por tu culpa, o se moverá una roca de su lugar?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
Porque la luz del pecador se apaga, y la llama de su fuego no brilla.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
La luz está oscura en su casa, y la luz que brilla sobre él se apaga.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Los pasos de su fuerza se vuelven cortos, y caerá en su propia trampa.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Sus pies lo llevan a la red, y él va caminando por las cuerdas.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Su pie es tomado en la red; él entra en su agarre.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
La cuerda se pone secretamente en la tierra para atraparlo, y la cuerda se coloca en su camino.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Lo superan los miedos por todos lados, lo persiguen a cada paso.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Su fuerza es debilitada por la necesidad de comida, y la destrucción está esperando su paso.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Su piel es desperdiciada por una enfermedad, le devora la carne poco a poco; él primogénito de la muerte.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Lo desarraigan de su tienda donde estaba a salvo, y se lo llevan al rey de los temores.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
En su tienda se verá lo que no es suyo, azufre se deja caer sobre su casa.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
Bajo la tierra, sus raíces están secas, y sobre ella se corta su rama.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Su memoria se ha ido de la tierra, y en las calles no hay conocimiento de su nombre.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
Él es enviado de la luz a la oscuridad; Él es obligado a salir del mundo.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
No tiene descendencia ni familia entre su pueblo, y en su lugar de residencia no hay nadie de su nombre.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
A su destino, los del oeste se sorprenden, y los del este son vencidos por el miedo.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
En verdad, estas son las casas del pecador, y este es el lugar de aquel que no tiene conocimiento de Dios.

< Ayubu 18 >