< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Y respondió Baldad Sujita, y dijo:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
¿Cuándo pondréis fin a las palabras? Entendéd, y después hablemos.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
¿Por qué somos tenidos por bestias? ¿en vuestros ojos, somos viles?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Oh tú que despedazas tu alma con tu furor, ¿será dejada la tierra por tu causa, y serán traspasadas las peñas de su lugar?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
Ciertamente la luz de los impíos será apagada, y la centella de su fuego no resplandecerá.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
La luz se oscurecerá en su tienda, y su candil se apagará sobre él.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Los pasos de su potencia serán acortados, y su mismo consejo le echará a perder.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Porque red será echada en sus pies, y sobre red andará.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Lazo prenderá su calcañar: esforzará contra él a los sedientos.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
Su cuerda está escondida en la tierra, y su orzuelo sobre la senda.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
De todas partes le asombrarán temores; y con sus mismos pies le ahuyentarán.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Su fuerza será hambrienta, y a su costilla estará aparejado quebrantamiento.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Comerá los ramos de su cuero, y el primogénito de la muerte tragará sus miembros.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Su confianza será arrancada de su tienda, y le harán llevar al rey de los espantos.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
En su misma tienda morará como si no fuese suya: piedrazufre será esparcida sobre su morada.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
Abajo se secarán sus raíces, y arriba serán cortados sus ramos.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Su memoria perecerá de la tierra, y no tendrá nombre por las calles.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
De la luz será lanzado a las tinieblas, y será echado del mundo.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
No tendrá hijo ni nieto en su pueblo, ni sucesor en sus moradas.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Sobre su día se espantarán los por venir, y a los antiguos tomarán pavor.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Ciertamente tales son las moradas del impío, y este es el lugar del que no conoció a Dios.

< Ayubu 18 >