< Ayubu 18 >
1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Entonces Bildad el Suhita respondió,
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
“¿Hasta cuándo vas a buscar palabras? Considera, y después hablaremos.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Por qué se nos cuenta como animales, que se han vuelto inmundos a tus ojos?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Tú que te desgarras en tu ira, ¿se abandonará la tierra por ti? ¿O la roca será removida de su lugar?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
“Sí, la luz de los impíos se apagará. La chispa de su fuego no brillará.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
La luz será oscura en su tienda. Su lámpara sobre él se apagará.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Los pasos de su fuerza se acortarán. Su propio consejo le hará caer.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Porque es arrojado a la red por sus propios pies, y se adentra en su malla.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Una trampa lo tomará por el talón. Una trampa lo atrapará.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
Un lazo está escondido para él en la tierra, una trampa para él en el camino.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Los terrores lo harán temer por todos lados, y le perseguirá los talones.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Su fuerza será famélica. Calamity estará listo a su lado.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Los miembros de su cuerpo serán devorados. El primogénito de la muerte devorará sus miembros.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Será desarraigado de la seguridad de su tienda. Será llevado ante el rey de los terrores.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
En su tienda habitará lo que no es suyo. El azufre será esparcido sobre su morada.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
Sus raíces se secarán por debajo. Su rama será cortada por encima.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Su memoria perecerá de la tierra. No tendrá nombre en la calle.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
Será expulsado de la luz a las tinieblas, y expulsado del mundo.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
No tendrá ni hijo ni nieto en su pueblo, ni que queden restos en el lugar donde vivía.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Los que vengan después se asombrarán de su día, como los que fueron antes se asustaron.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Ciertamente, tales son las moradas de los injustos. Este es el lugar del que no conoce a Dios”.