< Ayubu 18 >
1 Bildadi Mshuhi akajibu:
シユヒ人ビルダデこたへて曰く
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
汝等いつまで言語を獵求むることをするや 汝ら先曉るべし 然る後われら辨論はん
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
われら何ぞ獸畜とおもはるべけんや 何ぞ汝らの目に汚穢たる者と見らるべけんや
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
なんぢ怒りて身を裂く者よ 汝のためとて地あに棄られんや 磐あに其處より移されんや
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
惡き者の光明は滅され 其火の焔は照じ
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
その天幕の内なる光明は暗くなり其が上の燈火は滅さるべし
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
またその強き歩履は狹まり 其計るところは自分を陷いる
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
すなはち其足に逐れて網に到り また陷阱の上を歩むに
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
索はその踵に纒り 羂これを執ふ
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
索かれを執ふるために地に隱しあり 羂かれを陷しいるるために路に設けあり
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
怖ろしき事四方において彼を懼れしめ 其足にしたがひて彼をおふ
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
その力は餓ゑ 其傍には災禍そなはり
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
その膚の肢は蝕壞らる 即ち死の初子これが肢を蝕壞るなり
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
やがて彼はその恃める天幕より曳離されて懼怖の王の許に驅やられん
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
彼に屬せざる者かれの天幕に住み 硫礦かれの家の上に降ん
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
下にてはその根枯れ 上にてはその枝砍る
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
彼の跡は地に絶え 彼の名は街衢に傳はらじ
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
彼は光明の中より黑暗に逐やられ 世の中より驅出されん
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
彼はその民の中に子も無く孫も有じ また彼の住所には一人も遺る者なからん
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
之が日を見るにおいて後に來る者は駭ろき 先に出し者は怖おそれん
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
かならず惡き人の住所は是のごとく 神を知ざる者の所は是のごとくなるべし