< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Et Bildad, le Shukhite, répondit et dit:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
Jusques à quand tendrez-vous des pièges avec vos paroles? Soyez intelligents, et puis nous parlerons.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Pourquoi sommes-nous considérés comme des bêtes, et sommes-nous stupides à vos yeux?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Toi qui déchires ton âme dans ta colère, la terre sera-t-elle abandonnée à cause de toi, et le rocher sera-t-il transporté de sa place?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
Or la lumière des méchants sera éteinte, et la flamme de son feu ne luira point;
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
La lumière sera ténèbres dans sa tente, et sa lampe sera éteinte au-dessus de lui.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Les pas de sa force seront resserrés, et son propre conseil le renversera:
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Car il est poussé dans le filet par ses propres pieds; et il marche sur les mailles du filet;
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Le piège le prend par le talon, le lacet le saisit;
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
Sa corde est cachée dans la terre, et sa trappe sur le sentier.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
De toutes parts des terreurs l’alarment et le poussent çà et là, s’attachant à ses pas.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Sa force est affaiblie par la faim, et la calamité est prête à son côté.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Le premier-né de la mort dévore les membres de son corps, il dévore ses membres.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Ce qui faisait sa confiance est arraché de sa tente, et il est forcé de marcher vers le roi des terreurs.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
Ce qui n’est pas à lui habite dans sa tente, le soufre est répandu sur son habitation.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
En bas ses racines sèchent, et en haut ses branches sont coupées.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Sa mémoire périt de dessus la terre, et il n’a pas de nom sur la face du pays.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
Il est repoussé de la lumière dans les ténèbres; on le bannit du monde.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
Il n’a pas d’enfants ni de postérité parmi son peuple, personne qui lui survive dans les lieux de son séjour.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Ceux qui viennent après seront étonnés de son jour, comme l’horreur s’est emparée de ceux qui [les] ont précédés.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Certainement, telles sont les demeures de l’inique, et tel est le lieu de celui qui ne connaît pas Dieu.

< Ayubu 18 >