< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Et Bildad, le Shuhite, prit la parole,
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
« Combien de temps allez-vous chercher les mots? Réfléchissez, et après nous parlerons.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Pourquoi sommes-nous comptés comme des animaux, qui sont devenus impurs à vos yeux?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Toi qui te déchires dans ta colère, la terre sera-t-elle abandonnée pour vous? Ou bien la pierre sera-t-elle retirée de son emplacement?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
« Oui, la lumière des méchants sera éteinte. L'étincelle de son feu ne brillera pas.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
La lumière sera sombre dans sa tente. Sa lampe au-dessus de lui sera éteinte.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Les pas de sa force seront abrégés. Son propre conseil le fera tomber.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Car il est jeté dans un filet par ses propres pieds, et il s'égare dans ses mailles.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Un piège le saisit par le talon. Un piège va l'attraper.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
Un nœud coulant est caché pour lui dans le sol, un piège pour lui sur le chemin.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Des terreurs l'effraieront de toutes parts, et le poursuivra sur ses talons.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Sa force sera affamée. Calamity sera prêt à ses côtés.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Les membres de son corps seront dévorés. Le premier-né de la mort dévorera ses membres.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Il sera déraciné de la sécurité de sa tente. Il sera amené au roi des terreurs.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
Dans sa tente habitera ce qui n'est pas à lui. Le soufre sera répandu sur sa demeure.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
Ses racines seront desséchées par-dessous. Sa branche sera coupée en haut.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Son souvenir disparaîtra de la terre. Il n'aura pas de nom dans la rue.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
Il sera chassé de la lumière dans les ténèbres, et chassé du monde.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
Il n'aura ni fils ni petit-fils parmi son peuple, et aucun ne reste là où il a vécu.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Ceux qui viendront après seront étonnés de son jour, comme ceux qui les ont précédés ont été effrayés.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Telles sont les demeures des injustes. C'est la place de celui qui ne connaît pas Dieu. »

< Ayubu 18 >