< Ayubu 18 >
1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Odpovídaje pak Bildad Suchský, řekl:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
Dokudž neučiníte konce řečem? Pomyslte na to, a potom mluviti budeme.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Proč jsme počteni za hovada? Oškliví jsme jemu, jakž sami vidíte.
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
Ó ty, jenž hubíš život svůj zůřením svým, zdaliž pro tebe opuštěna bude země, a odsedne skála z místa svého?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
Anobrž světlo bezbožných uhašeno bude, aniž se blyštěti bude jiskra ohně jejich.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
Světlo se zatmí v stánku jeho, a lucerna jeho v něm zhasne.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
Ssouženi budou krokové síly jeho, a porazí jej rada jeho.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Nebo zapleten jest do síti nohami svými, a v zamotání chodí.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
Chytí ho za patu osídlo, a zmocní se ho násilník.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
Skrytať jest při zemi smečka jeho, a léčka jeho na stezce.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Odevšad hrůzy jej děsiti budou a dotírati na nohy jeho.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Hladovitá bude síla jeho, a bída pohotově při boku jeho.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
Zžíře žily kůže jeho, zžíře oudy jeho kníže smrti.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Uchváceno bude z stánku jeho doufání jeho, a to jej přivede k králi strachů.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
V stánku jeho hrůza bydleti bude, ač nebyl jeho; posypáno bude obydlí jeho sirou.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
Od zpodku kořenové jeho uschnou, a svrchu osekány budou ratolesti jeho.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
Památka jeho zahyne z země, aniž jméno jeho slýcháno bude na ulicích.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
Vyženou ho z světla do tmy, anobrž z okršlku zemského vypudí jej.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
Nepozůstaví ani syna ani vnuka v lidu svém, ani jakého ostatku v příbytcích svých.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
Nade dnem jeho zděsí se potomci, a přítomní strachem podjati budou.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Takovýť jest zajisté způsob nešlechetného, a takový cíl toho, kterýž nezná Boha silného.