< Ayubu 17 >

1 Moyo wangu umevunjika, siku zangu zimefupishwa, kaburi linaningojea.
わが霊は破れ、わが日は尽き、墓はわたしを待っている。
2 Hakika wenye mizaha wamenizunguka; macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.
まことにあざける者どもはわたしのまわりにあり、わが目は常に彼らの侮りを見る。
3 “Ee Mungu, nipe dhamana unayodai. Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?
どうか、あなた自ら保証となられるように。ほかにだれがわたしのために保証となってくれる者があろうか。
4 Umezifunga akili zao zisipate ufahamu, kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.
あなたは彼らの心を閉じて、悟ることのないようにされた。それゆえ、彼らに勝利を得させられるはずはない。
5 Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
分け前を得るために友を訴えるものは、その子らの目がつぶれるであろう。
6 “Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu, mtu ambaye watu humtemea mate usoni.
彼はわたしを民の笑い草とされた。わたしは顔につばきされる者となる。
7 Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi; umbile langu lote ni kama kivuli.
わが目は憂いによってかすみ、わがからだはすべて影のようだ。
8 Watu wanyofu wanatishwa na hili; watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.
正しい者はこれに驚き、罪なき者は神を信ぜぬ者に対して憤る。
9 Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao, nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.
それでもなお正しい者はその道を堅く保ち、潔い手をもつ者はますます力を得る。
10 “Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena! Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.
しかし、あなたがたは皆再び来るがよい、わたしはあなたがたのうちに賢い者を見ないのだ。
11 Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika, vivyo hivyo shauku za moyo wangu.
わが日は過ぎ去り、わが計りごとは敗れ、わが心の願いも敗れた。
12 Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana, kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’
彼らは夜を昼に変える。彼らは言う、『光が暗やみに近づいている』と。
13 Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, kama nikikitandika kitanda changu gizani, (Sheol h7585)
わたしがもし陰府をわたしの家として望み、暗やみに寝床をのべ、 (Sheol h7585)
14 kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’ na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’
穴に向かって『あなたはわたしの父である』と言い、うじに向かって『あなたはわたしの母、わたしの姉妹である』と言うならば、
15 liko wapi basi tarajio langu? Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?
わたしの望みはどこにあるか、だれがわたしの望みを見ることができようか。
16 Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? Je, tutashuka pamoja mavumbini?” (Sheol h7585)
これは下って陰府の関門にいたり、われわれは共にちりに下るであろうか」。 (Sheol h7585)

< Ayubu 17 >