< Ayubu 15 >
1 Kisha Elifazi Mtemani akajibu:
特曼人厄里法次又發言說:
2 “Je, mtu mwenye hekima hujibu kwa mawazo matupu, au kujaza tumbo lake kwa upepo wenye joto wa mashariki?
智者豈能以虛言作答﹖豈能以東風果腹﹖
3 Je, aweza kubishana juu ya maneno yasiyofaa, kwa hotuba zisizo na maana?
豈能以無益的廢話,無濟於事的言詞來辯護﹖
4 Lakini unadhoofisha hata uchaji wa Mungu na kuzuia ibada mbele za Mungu.
不但如此,而且你還廢除了敬畏天主之情,斷絕了在他面前的默禱。
5 Dhambi yako inasukuma kinywa chako, nawe umechagua ulimi wa hila.
其實,是你的罪惡教導你說話,叫你的口舌詭辯。
6 Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si changu; midomo yako mwenyewe inashuhudia dhidi yako.
定你罪的,是你的口而不是我,是你的口唇作證控告你。
7 “Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa? Ulizaliwa kabla ya vilima?
你豈是第一個出生的人﹖在山嶽未有之前,你豈已誕生﹖
8 Je, wewe husikiliza mashauri ya siri ya Mungu? Je, wewe unaizuia hekima iwe yako mwenyewe?
難道你聽見了天主的秘旨,把持著智慧﹖
9 Wewe unajua kitu gani tusichokijua sisi? Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
有什麼事,只有你知,而我們不知;只有你明瞭,而我們不明瞭﹖
10 Wale wenye mvi na wazee wako upande wetu, watu ambao ni wazee hata kuliko baba yako.
我們之中也有白頭老人,年紀比你父親還大。
11 Je, faraja za Mungu hazikutoshi, au maneno yaliyosemwa kwako kwa upole si kitu?
天主的安慰,和向你說的溫和的話,你以為還太少嗎﹖
12 Kwa nini moyo wako unakudanganya, na kwa nini macho yako yanangʼaa,
你為何讓你的感情控制著你﹖你的眼為何冒火,
13 ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu, na kumwaga maneno kama hayo kutoka kinywani mwako?
竟向天主發怒,開口說出這樣的話﹖
14 “Mwanadamu ni kitu gani, hata aweze kuwa safi, au yeye aliyezaliwa na mwanamke, hata aweze kuwa mwadilifu?
人算什麼而敢自稱潔淨,婦女所生的敢自稱正直﹖
15 Kama Mungu hawaamini watakatifu wake, kama hata mbingu zenyewe si safi machoni pake,
他連自己的聖者,還不信賴;在他眼中,連蒼天也不純潔,
16 sembuse mwanadamu ambaye ni mwovu na mpotovu, ambaye hunywa uovu kama anywavyo maji!
何況一個墮落可憎,飲惡如水的人。
17 “Nisikilize mimi nami nitakueleza, acha nikuambie yale niliyoyaona,
我要告訴你,你且聽我說;我要說明我的經驗,
18 ambayo watu wenye hekima wameyanena, bila kuficha lolote walilopokea toka kwa baba zao
即賢哲所傳授,和祖先未曾隱瞞的事:──
19 (wakati ambao wao peke yao ndio walipewa nchi, hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao):
這地方原只賜給了他們,尚無一個外方人從他們中間經過。──
20 Mtu mwovu siku zake zote hupata mateso, miaka yote aliwekewa mkorofi.
惡人一生飽受苦惱,壽數已給暴君限定;
21 Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake; katika kufanikiwa kwake, wanyangʼanyi humshambulia.
恐怖之聲常在他耳中,平靜時匪徒也來侵擾。
22 Hukata tamaa kuokoka gizani; amewekwa kwa ajili ya upanga.
他不相信還能脫離黑暗,只等待遭受刀劍之害,
23 Hutangatanga, akitafuta chakula; anajua kwamba siku ya giza iko karibu.
注定作為鷹鳥的食物,自知大難業已臨頭。
24 Taabu na maumivu makuu vinamtia hofu; humshinda kama mfalme aliye tayari kwa vita,
黑暗的日子使他恐怖,困苦艱難跟隨著他,好像準備廝殺的君王。
25 kwa sababu amemkunjia Mungu ngumi yake na kujigamba dhidi ya Mwenyezi,
因為他曾伸手反抗過天主,向全能者傲慢逞強過;
26 kwa kiburi akishambulia dhidi ya Mungu akiwa na ngao nene, iliyo imara.
以伸直的頸項,以堅厚的盾背攻擊過天主。
27 “Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene na kiuno chake kimevimba kwa kunenepa,
他的臉蓋滿了脂油,他的腰積滿了肥肉。
28 ataishi katika miji ya magofu, na katika nyumba ambazo haziishi mwanadamu yeyote, nyumba zinazokuwa vifusi.
他住在荒涼的城內,住在無人居留,行將化為廢墟的屋中。
29 Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu, wala mali zake hazitakuwa nyingi juu ya nchi.
他不能富有,所有的財富也不能久存,也決不能向地下生根。
30 Hatatoka gizani; mwali wa moto utanyausha machipukizi yake, nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.
他脫離不了黑暗,火燄要灼乾他的嫩芽,暴風要吹去他的花朵。
31 Asijidanganye mwenyewe kutumainia ubatili, kwa kuwa hatapata malipo yoyote.
別依恃枝椏已長大,應知這都是空虛;
32 Atakuwa amelipwa kikamilifu kabla ya wakati wake, nayo matawi yake hayatastawi.
未到時日,已經凋謝,枝葉再不發綠。
33 Atafanana na mzabibu uliopukutishwa matunda yake kabla hayajaiva, kama mzeituni unaodondosha maua yake.
有如葡萄未熟即被打下,橄欖開花即被搖落,
34 Kwa kuwa jamii ya wasiomcha Mungu watakuwa tasa, nao moto utateketeza hema za wale wanaopenda rushwa.
因為惡人的家室必要絕嗣,火要燒盡受賄者的帳幕。
35 Hutunga mimba ya madhara na kuzaa uovu; matumbo yao huumba udanganyifu.”
他們所懷的是邪惡,所生的是罪孽;心胸懷念的,無非是欺詐。