< Ayubu 14 >
1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
EL HOMBRE nacido de mujer, corto de días, y harto de sinsabores:
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
Que sale como una flor y es cortado; y huye como la sombra, y no permanece.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
¿Y sobre éste abres tus ojos, y me traes á juicio contigo?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
¿Quién hará limpio de inmundo? Nadie.
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
Ciertamente sus días están determinados, y el número de sus meses está cerca de ti: tú le pusiste términos, de los cuales no pasará.
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
Si tú lo dejares, él dejará [de ser]: entre tanto deseará, como el jornalero, su día.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
Porque si el árbol fuere cortado, aun queda de él esperanza; retoñecerá aún, y sus renuevos no faltarán.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
Si se envejeciere en la tierra su raíz, y su tronco fuere muerto en el polvo,
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
Al percibir el agua reverdecerá, y hará copa como planta.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
Mas el hombre morirá, y será cortado; y perecerá el hombre, ¿y dónde estará él?
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
Las aguas de la mar se fueron, y agotóse el río, secóse.
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
Así el hombre yace, y no se tornará á levantar: hasta que no haya cielo no despertarán, ni se levantarán de su sueño.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol )
¡Oh quién me diera que me escondieses en el sepulcro, que me encubrieras hasta apaciguarse tu ira, que me pusieses plazo, y de mí te acordaras! (Sheol )
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
Si el hombre muriere, ¿[volverá] á vivir? Todos los días de mi edad esperaré, hasta que venga mi mutación.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
Aficionado á la obra de tus manos, llamarás, y yo te responderé.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
Pues ahora me cuentas los pasos, y no das tregua á mi pecado.
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
Tienes sellada en saco mi prevaricación, y coacervas mi iniquidad.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
Y ciertamente el monte que cae se deshace, y las peñas son traspasadas de su lugar;
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
Las piedras son desgastadas con el agua impetuosa, que se lleva el polvo de la tierra: de tal manera haces tú perecer la esperanza del hombre.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
Para siempre serás más fuerte que él, y él se va; demudarás su rostro, y enviaráslo.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
Sus hijos serán honrados, y él no lo sabrá; ó serán humillados, y no entenderá de ellos.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
Mas su carne sobre él se dolerá, y entristecerse ha en él su alma.