< Ayubu 14 >

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
El hombre nacido de mujer es corto de días y lleno de perturbaciones.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
Brota como una flor, pero es cortado. Pasa como una sombra y desaparece.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
¿Y sobre éste abres tus ojos y lo llevas a juicio contigo?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
¿Quién limpiará lo impuro? ¡Nadie!
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
Ciertamente sus días están determinados, y el número de sus meses depende de Ti. Tú le fijaste sus límites, de los cuales no pasará.
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
Aparta de él tu mirada y que descanse hasta que complete su día como un jornalero.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
Porque para el árbol hay esperanza: Si es cortado, retoñará, y sus ramas no cesarán.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
Aunque debajo de la tierra esté muerto su tronco, y en la tierra envejezca su raíz,
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
al recibir el agua reverdecerá, y echará ramas como una planta.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
Pero el hombre muere, y queda tendido. Expira el hombre, ¿y dónde está?
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
Como las aguas se van al mar, y un río se agota y se seca,
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
así el hombre queda tendido y no se levantará. Hasta que no haya cielo, no será despertado, ni lo levantarán de su sueño.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
¡Ojalá me escondas en el Seol mientras se aplaca tu ira, y me fijes un plazo y te acuerdes de mí! (Sheol h7585)
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
Si el hombre muere, ¿volverá a vivir? Todos los días de mi lucha y servicio esperaré hasta que llegue mi liberación.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
Entonces llamarás y yo te responderé. Tendrás afecto a la hechura de tus manos.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
Porque ahora me cuentas los pasos y no das tregua a mi pecado.
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
Tienes mi transgresión sellada en un saco. Tú cubres mi iniquidad.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
Pero la montaña cae y se desmorona. Las rocas cambian de lugar.
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
Las piedras se desgastan con el agua impetuosa que se lleva el polvo de la tierra. Así destruyes la esperanza del hombre.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
Prevaleces para siempre contra él, y él se va. Desfiguras su rostro y lo despides.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
Sus hijos obtendrán honores, pero él no lo sabrá. Si son humillados, no lo percibirá.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
Pero su carne sobre él siente el tormento, y su alma gime por él.

< Ayubu 14 >