< Ayubu 14 >

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
A human being born of a woman [is] short of days and surfeited of turmoil.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
Like a flower he comes forth and he withered and he fled like shadow and not he remains.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
Indeed? on this do you open eyes your and me do you bring? in judgment with yourself.
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
Who? will he make a clean [thing] from an unclean [thing] not one [person].
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
If [are] determined - days his [the] number of months his [is] with you (limits his *Q(K)*) you have appointed and not he will pass.
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
Look away from on him so he may cease until he takes pleasure in like a hired laborer day his.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
For there for a tree [is] hope if it will be cut down and again it will sprout afresh and young shoot[s] its not it will fail.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
Though it will grow old in the ground root its and in the dust it will die stump its.
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
From [the] scent of water it will show buds and it will produce shoot[s] like a plant.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
And a man he dies and he was weak and he expired a person and where [is]? he.
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
They disappear waters from [the] sea and a river it dries up and it is dry.
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
And a person he lies down and not he will arise until [is] not heaven not they will awake and not they will be roused from sleep their.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
Who? will he give - in Sheol you will hide me you will conceal me until turns back anger your you will set for me a limit and you will remember me. (Sheol h7585)
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
If he will die a man ¿ will he live all [the] days of service my I will wait until comes relief my.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
You will call and I I will answer you for [the] work of hands your you will long.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
For now steps my you will count not you will watch over sin my.
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
[will be] sealed up In a bag transgression my and you have smeared over iniquity my.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
And but a mountain [is] falling it crumbles away and a rock it moves from place its.
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
Stones - they rub away waters it washes off overflowings its [the] dust of [the] earth and [the] hope of humankind you destroy.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
You overpower him to perpetuity and he went [you are] changing face his and you sent away him.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
They are honored sons his and not he knows and they may be insignificant and not he perceives it.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
Only own flesh his on himself it is in pain and self his on himself it mourns.

< Ayubu 14 >