< Ayubu 14 >

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
Man born of a woman is short of days, and sated with harrowing trouble.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
Like a flower he cometh forth, and is cut down: and he fleeth like a shadow, and remaineth not.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
And yet on such a one dost thou open thy eyes, and me thou bringest into judgment with thee?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
Who can make a clean thing out of an unclean? not one [thing].
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
Seeing that his days are determined, the number of his months are [fixed] with thee, that thou hast set his bounds which he cannot pass:
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
Turn thyself from him that he may recover from his pain, and be able to enjoy like a hired laborer his day.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
For there is hope for the tree: if it be cut down, it may still sprout again, while its young shoot will not cease.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
If even its root become old in the earth, and its stock die in the dust:
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
Yet through the scent of water will it flourish [again], and produce boughs as though It were newly planted.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
But man dieth, and lieth powerless: yea, the son of earth departeth—and where is he?
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
The waters run off from the sea, and the river faileth and drieth up:
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
So doth man lie down, and riseth not: till the heavens be no more, they will not awake, and will not be roused out of their sleep.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
Oh who would grant that thou mightest hide me in the nether world, that thou mightest conceal me, until thy wrath be appeased, that thou mightest set for me a fixed time, and remember me then! (Sheol h7585)
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
Or, when a man dieth, will he live again? all the days of my time of service would I then wait, till [the hour of] my release were come.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
Do thou call, and I will truly answer thee: have a desire for the work of thy hands.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
Yet now thou numberest my steps: and thou waitest not with [the punishment of] my sin.
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
Sealed up in a bag is my transgression, and thou yet addest to my iniquity.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
But truly a falling mountain will crumble, and [even] a rock is moved out of its place.
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
The water weareth out stones; thou sweepest away their fragments [like] the dust of the earth: and so thou destroyest the hope of man.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
Thou assailest him with might without ceasing, till he passeth away: thou changest his countenance, and sendest him off.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
His children acquire honor, but he knoweth it not: and they are esteemed little, but he perceiveth nothing of them.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
But his body. on him, feeleth pain, and his soul will mourn for him.

< Ayubu 14 >