< Ayubu 14 >

1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
Man that is born of a woman is of few days, and full of trouble.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
He cometh forth like a flower, and withereth; he fleeth also as a shadow, and continueth not.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
And dost Thou open Thine eyes upon such a one, and bringest me into judgment with Thee?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
Who can bring a clean thing out of an unclean? not one.
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
Seeing his days are determined, the number of his months is with Thee, and Thou hast appointed his bounds that he cannot pass;
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
Look away from him, that he may rest, till he shall accomplish, as a hireling, his day.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
For there is hope of a tree, if it be cut down, that it will sprout again, and that the tender branch thereof will not cease.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
Though the root thereof wax old in the earth, and the stock thereof die in the ground;
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
Yet through the scent of water it will bud, and put forth boughs like a plant.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
But man dieth, and lieth low; yea, man perisheth, and where is he?
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
As the waters fail from the sea, and the river is drained dry;
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
So man lieth down and riseth not; till the heavens be no more, they shall not awake, nor be roused out of their sleep.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
Oh that Thou wouldest hide me in the nether-world, that Thou wouldest keep me secret, until Thy wrath be past, that Thou wouldest appoint me a set time, and remember me! — (Sheol h7585)
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
If a man die, may he live again? All the days of my service would I wait, till my relief should come —
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
Thou wouldest call, and I would answer Thee; Thou wouldest have a desire to the work of Thy hands.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
But now Thou numberest my steps, Thou dost not even wait for my sin;
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
My transgression is sealed up in a bag, and Thou heapest up mine iniquity.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
And surely the mountain falling crumbleth away, and the rock is removed out of its place;
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
The waters wear the stones; the overflowings thereof wash away the dust of the earth; so Thou destroyest the hope of man.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
Thou prevailest for ever against him, and he passeth; Thou changest his countenance, and sendest him away.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
His sons come to honour, and he knoweth it not; and they are brought low, but he regardeth them not.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
But his flesh grieveth for him, and his soul mourneth over him.

< Ayubu 14 >