< Ayubu 14 >
1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
Čovjek koga je žena rodila kratka je vijeka i pun nevolja.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
K'o cvijet je nikao i vene već, poput sjene bježi ne zastajuć'.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
Na takva, zar, ti oči otvaraš i preda se na sud ga izvodiš?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
Tko će čisto izvuć' iz nečista? Nitko!
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
Pa kad su njegovi dani odbrojeni, kad mu broj mjeseci o tebi ovisi, kad mu granicu stavljaš neprijelaznu,
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
skini s njega pogled da počinut' može, poput najamnika da svoj dan uživa.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
TÓa ni drvu nije nada sva propala, posječeno, ono opet prozeleni i mladice nove iz njega izbiju.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
Ako mu korijen i ostari u zemlji, ako mu se panj i sasuši u prahu,
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
oćutjevši vodu, ono će propupat' i pustiti grane kao stablo novo.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
Al' kad čovjek umre, ostaje pokošen, kad smrtnik izdahne, gdje li je on tada?
11 Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
Može sva voda iz mora ispariti i presahnut' rijeke, isušit posvema',
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
al' čovjek kad legne, ne ustaje više, dok nebesa bude, neće se podići, od sna se svojega probuditi neće.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol )
O, kad bi me htio skriti u Šeolu, zakloniti me dok srdžba ti ne mine, dÓati mi rok kad ćeš me se spomenuti, (Sheol )
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
- jer, kad umre čovjek, zar uskrsnut' može? - čekao bih te sve dane vojske svoje dok ne bi došao da mi smjenu dadeš.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
Zvao bi me, a ja bih se odazvao: zaželio si se djela svojih ruku.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
A sad nad svakim mojim vrebaš korakom, nijednog mi grijeha nećeš oprostiti,
17 Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
u vreći si prijestup moj zapečatio i krivicu moju svu si zapisao.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
Vaj! K'o što se jednom uruši planina, k'o što se hridina s mjesta svog odvali,
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
k'o što voda kamen s vremenom istroši, a pljusak bujicom zemlju svu sapere, tako uništavaš nadu u čovjeku.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
Oborio si ga - on ode za svagda, nagrđena lica, otjeran, odbačen.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
Djecu mu poštuju - o tom ništa ne zna; ako su prezrena - o tom ne razmišlja.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
On jedino pati zbog svojega tijela, on jedino tuži zbog svojeg života.”