< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
HE AQUÍ que todas estas cosas han visto mis ojos, y oído y entendido de por sí mis oídos.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Como vosotros lo sabéis, lo sé yo; no soy menos que vosotros.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Mas yo hablaría con el Todopoderoso, y querría razonar con Dios.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Que ciertamente vosotros sois fraguadores de mentira; sois todos vosotros médicos nulos.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Ojalá callarais del todo, porque os fuera sabiduría.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Oid ahora mi razonamiento, y estad atentos á los argumentos de mis labios.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
¿Habéis de hablar iniquidad por Dios? ¿habéis de hablar por él engaño?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
¿Habéis de hacer acepción de su persona? ¿habéis de pleitear vosotros por Dios?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
¿Sería bueno que él os escudriñase? ¿os burlaréis de él como quien se burla de algún hombre?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
El os reprochará de seguro, si solapadamente hacéis acepción de personas.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
De cierto su alteza os había de espantar, y su pavor había de caer sobre vosotros.
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Vuestras memorias serán comparadas á la ceniza, y vuestros cuerpos como cuerpos de lodo.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Escuchadme, y hablaré yo, y véngame después lo que viniere.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
¿Por qué quitaré yo mi carne con mis dientes, y pondré mi alma en mi mano?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
He aquí, aunque me matare, en él esperaré; empero defenderé delante de él mis caminos.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Y él mismo me será salud, porque no entrará en su presencia el hipócrita.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Oid con atención mi razonamiento, y mi denunciación con vuestros oídos.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
He aquí ahora, si yo me apercibiere á juicio, sé que seré justificado.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
¿Quién es el que pleiteará conmigo? porque si ahora yo callara, fenecería.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
A lo menos dos cosas no hagas conmigo; entonces no me esconderé de tu rostro:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Aparta de mí tu mano, y no me asombre tu terror.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Llama luego, y yo responderé; ó yo hablaré, y respóndeme tú.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
¿Cuántas iniquidades y pecados tengo yo? hazme entender mi prevaricación y mi pecado.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
¿Por qué escondes tu rostro, y me cuentas por tu enemigo?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
¿A la hoja arrebatada has de quebrantar? ¿y á una arista seca has de perseguir?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
¿Por qué escribes contra mí amarguras, y me haces cargo de los pecados de mi mocedad?
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Pones además mis pies en el cepo, y guardas todos mis caminos, imprimiéndolo á las raíces de mis pies.
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Y el [cuerpo mío] se va gastando como de carcoma, como vestido que se come de polilla.

< Ayubu 13 >