< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
[Ecce omnia hæc vidit oculus meus, et audivit auris mea, et intellexi singula.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Secundum scientiam vestram et ego novi: nec inferior vestri sum.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Sed tamen ad Omnipotentem loquar, et disputare cum Deo cupio:
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
prius vos ostendens fabricatores mendacii, et cultores perversorum dogmatum.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Atque utinam taceretis, ut putaremini esse sapientes.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Audite ergo correptionem meam, et judicium labiorum meorum attendite.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Numquid Deus indiget vestro mendacio, ut pro illo loquamini dolos?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
numquid faciem ejus accipitis, et pro Deo judicare nitimini?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
aut placebit ei quem celare nihil potest? aut decipietur, ut homo, vestris fraudulentiis?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Ipse vos arguet, quoniam in abscondito faciem ejus accipitis.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Statim ut se commoverit, turbabit vos, et terror ejus irruet super vos.
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Memoria vestra comparabitur cineri, et redigentur in lutum cervices vestræ.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Tacete paulisper, ut loquar quodcumque mihi mens suggesserit.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Quare lacero carnes meas dentibus meis, et animam meam porto in manibus meis?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Etiam si occiderit me, in ipso sperabo: verumtamen vias meas in conspectu ejus arguam.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Et ipse erit salvator meus: non enim veniet in conspectu ejus omnis hypocrita.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Audite sermonem meum, et ænigmata percipite auribus vestris.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Si fuero judicatus, scio quod justus inveniar.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Quis est qui judicetur mecum? veniat: quare tacens consumor?
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Duo tantum ne facias mihi, et tunc a facie tua non abscondar:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
manum tuam longe fac a me, et formido tua non me terreat.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Voca me, et ego respondebo tibi: aut certe loquar, et tu responde mihi.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Quantas habeo iniquitates et peccata? scelera mea et delicta ostende mihi.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Cur faciem tuam abscondis, et arbitraris me inimicum tuum?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Contra folium, quod vento rapitur, ostendis potentiam tuam, et stipulam siccam persequeris:
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
scribis enim contra me amaritudines, et consumere me vis peccatis adolescentiæ meæ.
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Posuisti in nervo pedem meum, et observasti omnes semitas meas, et vestigia pedum meorum considerasti:
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
qui quasi putredo consumendus sum, et quasi vestimentum quod comeditur a tinea.]