< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
視よわが目これを盡く觀 わが耳これを聞て通逹れり
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
汝らが知るところは我もこれを知る 我は汝らに劣らず
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
然りと雖ども我は全能者に物言ん 我は神と論ぜんことをのぞむ
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
汝らは只謊言を造り設くる者 汝らは皆無用の醫師なり
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
願くは汝ら全く默せよ 然するは汝らの智慧なるべし
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
請ふわが論ずる所を聽き 我が唇にて辨爭そふ所を善く聽け
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
神のために汝ら惡き事を言や 又かれのために虚僞を述るや
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
汝ら神の爲に偏るや またかれのために爭はんとするや
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
神もし汝らを鑒察たまはば豈善らんや 汝等人を欺むくごとくに彼を欺むき得んや
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
汝等もし密に私しするあらば彼かならず汝らを責ん
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
その威光なんぢらを懼れしめざらんや 彼を懼るる畏懼なんぢらに臨まざらんや
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
なんぢらの諭言は灰に譬ふべし なんぢらの城は土の城となる
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
默して我にかかはらざれ 我言語んとす 何事にもあれ我に來らば來れ
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
我なんぞ我肉をわが齒の間に置き わが生命をわが手に置かんや
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
彼われを殺すとも我は彼に依頼まん 唯われは吾道を彼の前に明かにせんとす
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
彼また終に我救拯とならん 邪曲なる者は彼の前にいたること能はざればなり
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
なんぢら聽よ 我言を聽け我が述る所をなんぢらの耳に入しめよ
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
視よ我すでに吾事を言竝べたり 必ず義しとせられんと自ら知る
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
誰か能くわれと辨論ふ者あらん 若あらば我は口を緘て死ん
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
惟われに二の事を爲たまはざれ 然ば我なんぢの面をさけて隱れじ
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
なんぢの手を我より離したまへ 汝の威嚴をもて我を懼れしめたまはざれ
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
而して汝われを召したまへ 我こたへん 又われにも言はしめて汝われに答へたまへ
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
我の愆われの罪いくばくなるや 我の背反と罪とを我に知しめたまへ
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
何とて御顏を隱し我をもて汝の敵となしたまふや
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
なんぢは吹廻さるる木の葉を威し 干あがりたる籾殼を追ひたまふや
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
汝は我につきて苦き事等を書しるし 我をして我が幼稚時の罪を身に負しめ
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
わが足を足械にはめ 我すべての道を伺ひ我足の周圍に限界をつけたまふ
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
我は腐れたる者のごとくに朽ゆき 蠹に食るる衣服に等し