< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Ecco, tutto questo ha visto il mio occhio, l'ha udito il mio orecchio e l'ha compreso.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Quel che sapete voi, lo so anch'io; non sono da meno di voi.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Ma io all'Onnipotente vorrei parlare, a Dio vorrei fare rimostranze.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Voi siete raffazzonatori di menzogne, siete tutti medici da nulla.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Magari taceste del tutto! sarebbe per voi un atto di sapienza!
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Ascoltate dunque la mia riprensione e alla difesa delle mie labbra fate attenzione.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Volete forse in difesa di Dio dire il falso e in suo favore parlare con inganno?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Vorreste trattarlo con parzialità e farvi difensori di Dio?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Sarebbe bene per voi se egli vi scrutasse? Come s'inganna un uomo, credete di ingannarlo?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Severamente vi redarguirà, se in segreto gli siete parziali.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Forse la sua maestà non vi incute spavento e il terrore di lui non vi assale?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Sentenze di cenere sono i vostri moniti, difese di argilla le vostre difese.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Tacete, state lontani da me: parlerò io, mi capiti quel che capiti.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Voglio afferrare la mia carne con i denti e mettere sulle mie mani la mia vita.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Mi uccida pure, non me ne dolgo; voglio solo difendere davanti a lui la mia condotta!
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Questo mi sarà pegno di vittoria, perché un empio non si presenterebbe davanti a lui.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Ascoltate bene le mie parole e il mio esposto sia nei vostri orecchi.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Ecco, tutto ho preparato per il giudizio, son convinto che sarò dichiarato innocente.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Chi vuol muover causa contro di me? Perché allora tacerò, pronto a morire.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Solo, assicurami due cose e allora non mi sottrarrò alla tua presenza;
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
allontana da me la tua mano e il tuo terrore più non mi spaventi;
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
poi interrogami pure e io risponderò oppure parlerò io e tu mi risponderai.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Quante sono le mie colpe e i miei peccati? Fammi conoscere il mio misfatto e il mio peccato.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Perché mi nascondi la tua faccia e mi consideri come un nemico?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Vuoi spaventare una foglia dispersa dal vento e dar la caccia a una paglia secca?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
Poiché scrivi contro di me sentenze amare e mi rinfacci i miei errori giovanili;
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
tu metti i miei piedi in ceppi, spii tutti i miei passi e ti segni le orme dei miei piedi.
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Intanto io mi disfò come legno tarlato o come un vestito corroso da tignola.