< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
»Seht, dies alles hat mein Auge gesehen, hat mein Ohr gehört und es sich gemerkt.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Soviel ihr wißt, weiß ich auch: ich stehe hinter euch nicht zurück.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Doch ich will zum Allmächtigen reden und trage Verlangen, mich mit Gott auseinanderzusetzen.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Ihr dagegen seid nur Lügenschmiede, Pfuscherärzte allesamt.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
O wolltet ihr doch ganz stille schweigen: das würde euch als Weisheit angerechnet werden.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Hört doch meine Rechtfertigung an und achtet auf die Entgegnungen meiner Lippen!
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Wollt ihr Gott zur Ehre Lügen reden und ihm zuliebe Trug vorbringen?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Wollt ihr Parteilichkeit zu seinen Gunsten üben oder Gottes Sachwalter spielen?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Würde es gut für euch ablaufen, wenn er euch ins Verhör nimmt, oder könnt ihr ihn narren, wie man Menschen narrt?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Mit aller Strenge wird er euch strafen, wenn ihr im geheimen Partei (für ihn) ergreift.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Wird nicht sein bloßes Sich-Erheben euch fassungslos machen und Schrecken vor ihm euch befallen?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Eure Denksprüche sind Sprüche so lose wie Asche, eure Schanzen erweisen sich als Schanzen von Lehm!«
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
»So schweigt denn vor mir still: ich will reden, es mag über mich hereinfahren, was da will!
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Warum sollte ich mein Fleisch in meinen Zähnen forttragen und meine Seele in meine offene Hand legen?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Er wird mich ja doch töten, ich habe auf nichts mehr zu hoffen; nur meinen bisherigen Wandel will ich offen vor ihm darlegen.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Schon das muß mir zugute kommen, denn kein Heuchler darf ihm vor die Augen treten.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
So hört denn meine Rede aufmerksam an und laßt meine Darlegung in euer Ohr dringen!
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Seht doch: ich bin zum Rechtsstreit gerüstet! Ich weiß, daß ich, ja ich, recht behalten werde.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Wer ist es, der mit mir rechten dürfte? Denn in diesem Fall wollte ich lieber verstummen und den Tod erleiden!
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Nur zweierlei tu mir dabei nicht an (o Gott), dann will ich mich vor deinem Angesicht nicht verbergen:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
ziehe deine Hand von mir zurück und laß deine schreckliche Erscheinung mich nicht ängstigen!
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Dann rufe mich, so will ich mich verantworten; oder ich will reden, und du entgegne mir!«
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
»Wie viele Übertretungen und Missetaten habe ich (begangen)? Meine Übertretung und meine Sünde laß mich wissen!
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Warum verbirgst du dein Angesicht vor mir und siehst in mir deinen Feind?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Willst du ein verwehtes Blatt noch aufschrecken und einem dürren Strohhalm noch nachjagen,
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
daß du mir so bittere Arzneien verschreibst und mich sogar die Verfehlungen meiner Jugend büßen läßt?
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Daß du meine Füße in den Block legst und alle meine Pfade überwachst, meinen Füßen jede freie Bewegung entziehst,
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
mir, einem Manne, der wie ein vom Wurm zerfressenes Gerät zerfällt, wie ein Kleid, das die Motten zernagt haben?«

< Ayubu 13 >