< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Siehe, das alles hat mein Auge gesehen und mein Ohr gehört, und ich habe es verstanden.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Was ihr wißt, das weiß ich auch; und bin nicht geringer denn ihr.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Doch wollte ich gern zu dem Allmächtigen reden und wollte gern mit Gott rechten.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Aber ihr deutet's fälschlich und seid alle unnütze Ärzte.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Wollte Gott, ihr schwieget, so wäret ihr weise.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Höret doch meine Verantwortung und merket auf die Sache, davon ich rede!
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Wollt ihr Gott verteidigen mit Unrecht und für ihn List brauchen?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Wollt ihr seine Person ansehen? Wollt ihr Gott vertreten?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Wird's euch auch wohl gehen, wenn er euch richten wird? Meint ihr, daß ihr ihn täuschen werdet, wie man einen Menschen täuscht?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Er wird euch strafen, wo ihr heimlich Person ansehet.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Wird er euch nicht erschrecken, wenn er sich wird hervortun, und wird seine Furcht nicht über euch fallen?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Eure Denksprüche sind Aschensprüche; eure Bollwerke werden wie Lehmhaufen sein.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Schweiget mir, daß ich rede, es komme über mich, was da will.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Was soll ich mein Fleisch mit meinen Zähnen davontragen und meine Seele in meine Hände legen?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Siehe, er wird mich doch erwürgen, und ich habe nichts zu hoffen; doch will ich meine Wege vor ihm verantworten.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Er wird ja mein Heil sein; denn es kommt kein Heuchler vor ihn.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Höret meine Rede, und meine Auslegung gehe ein zu euren Ohren.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Siehe, ich bin zum Rechtsstreit gerüstet; ich weiß, daß ich recht behalten werde.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Wer ist, der mit mir rechten könnte? Denn dann wollte ich schweigen und verscheiden.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Zweierlei tue mir nur nicht, so will ich mich vor dir nicht verbergen:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
laß deine Hand fern von mir sein, und dein Schrecken erschrecke mich nicht!
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Dann rufe, ich will antworten, oder ich will reden, antworte du mir!
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Wie viel ist meiner Missetaten und Sünden? Laß mich wissen meine Übertretung und Sünde.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Warum verbirgst du dein Antlitz und hältst mich für deinen Feind?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Willst du wider ein fliegend Blatt so ernst sein und einen dürren Halm verfolgen?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
Denn du schreibst mir Betrübnis an und willst über mich bringen die Sünden meiner Jugend.
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Du hast meinen Fuß in den Stock gelegt und hast acht auf alle meine Pfade und siehst auf die Fußtapfen meiner Füße,
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
der ich doch wie Moder vergehe und wie ein Kleid, das die Motten fressen.

< Ayubu 13 >