< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Sieh', alles hat mein Auge gesehen, mein Ohr gehört und sich's gemerkt!
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Was ihr wißt, weiß ich auch; ich stehe hinter euch nicht zurück.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Aber ich will zum Allmächtigen reden und mit Gott zu rechten habe ich Lust.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Denn wahrlich, ihr seid Lügenschmiede und Flicker von Nichtigem insgesamt.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
O daß ihr doch ganz stille schwiegt, so könnte das als eure Weisheit gelten!
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
So hört denn die Rüge meines Mundes und merkt auf die Vorwürfe meiner Lippen.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Wollt ihr Gott zu Liebe Unrecht reden und ihm zu Liebe Trug reden?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Wollt ihr für ihn Partei ergreifen oder für Gott streiten?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Wird es gut ablaufen, wenn er euch erforscht, oder wollt ihr ihn narren, wie man Menschen narrt?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Nein, strafen, strafen wird er euch, wenn ihr insgeheim Partei ergreift.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Seine Hoheit wird euch betäuben, und sein Schrecken auf euch fallen.
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Eure Merksprüche sind Aschensprüche, Lehmschanzen sind eure Schanzen.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Laßt mich in Ruhe, so will ich reden, mag über mich ergehen, was da will.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Ich will mein Fleisch in meine Zähne nehmen und mein Leben aufs Spiel setzen.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Er wird mich töten - ich harre seiner; nur will ich meinen Wandel ihm ins Angesicht darlegen.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Schon das gereicht mir zum Sieg, daß vor sein Angesicht kein Heuchler tritt.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
So hört denn aufmerksam meine Rede, und meine Darlegung dringe zu euren Ohren.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Wohlan, ich habe den Handel eingeleitet; ich weiß, daß ich Recht behalten werde.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Wer ist's, der mit mir streiten dürfte? - denn dann wollt' ich schweigen und verscheiden!
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Nur zweierlei thue mir nicht an, dann will ich mich vor deinem Antlitz nicht verbergen:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Zieh deine Hand von mir zurück und laß deinen Schrecken mich nicht ängstigen;
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
dann rufe, so will ich Rede stehn, oder ich will reden, und du entgegne mir!
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Wieviel Vergehungen und Sünden habe ich denn? Meinen Frevel und meine Sünde laß mich wissen!
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Warum verhüllst du dein Antlitz und erachtest mich für deinen Feind?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Willst du ein verwehtes Blatt aufschrecken und den dürren Halm verfolgen,
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
daß du mir Bitteres als Urteil schreibst und mich die Sünden meiner Jugend erben lässest?
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
daß du meine Füße in den Block legst und alle meine Wege bewachst und dir einen Kreis um meine Sohlen ziehst?
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Und eben dieser Mann zerfällt wie von Wurmfraß, wie ein Kleid, das die Motte zerfressen hat!

< Ayubu 13 >