< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Voici, mon œil a vu tout cela; mon oreille l'a entendu et compris;
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Ce que vous savez, je le sais aussi; je ne vous suis pas inférieur.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Mais je veux parler au Tout-Puissant, je veux plaider auprès de Dieu.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Mais vous, vous êtes des inventeurs de mensonges. Vous êtes tous des médecins de néant.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Puissiez-vous demeurer dans le silence, et que ce soit là votre sagesse!
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Écoutez donc ma réprimande, et soyez attentifs à la réplique de mes lèvres.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Tiendrez-vous des discours injustes en faveur de Dieu? Et, pour le défendre, direz-vous des mensonges?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Ferez-vous acception de personnes en sa faveur? Prétendrez-vous plaider pour Dieu?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Vous en prendra-t-il bien, s'il vous sonde? Comme on trompe un homme, le tromperez-vous?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Certainement, il vous reprendra, si secrètement vous faites acception de personnes.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Sa majesté ne vous épouvantera-t-elle point, et sa frayeur ne tombera-t-elle pas sur vous?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Vos réminiscences sont des sentences de cendre, vos remparts sont des remparts de boue!
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Taisez-vous, laissez-moi; je veux parler, et qu'il m'arrive ce qui pourra.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Pourquoi prendrais-je ma chair dans mes dents? Non, j'exposerai ma vie.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Voici, il me tuera; je n'ai plus d'espoir. Du moins, je défendrai ma conduite devant lui.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Et cela me tournera à salut; car un impie ne viendrait pas devant lui.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Écoutez, écoutez mes paroles, prêtez l'oreille à mes déclarations.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Voici, j'ai préparé ma cause. Je sais que je serai justifié.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Quelqu'un plaidera-t-il contre moi? Alors je me tais, et je meurs.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Seulement, ne me fais point deux choses, et alors je ne me cacherai pas loin de ta face:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Éloigne ta main de moi, et que ta terreur ne me trouble point.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Puis, appelle-moi et je répondrai. Ou bien, que je parle, et tu me répliqueras.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Combien ai-je commis d'iniquités et de péchés? Fais-moi connaître ma transgression et mon péché.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Pourquoi caches-tu ta face, et me tiens-tu pour ton ennemi?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Veux-tu effrayer une feuille que le vent emporte, et poursuivre une paille desséchée?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
Pour que tu écrives contre moi d'amers arrêts, et que tu me fasses recevoir la peine des péchés de ma jeunesse;
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Pour que tu mettes mes pieds dans des ceps, que tu épies tous mes chemins, et que tu traces une limite autour de la plante de mes pieds;
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Et ce corps se détruit comme du bois vermoulu, comme un vêtement que la teigne a rongé.