< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Voici, mon œil a vu tout cela, Mon oreille l’a entendu et y a pris garde.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Ce que vous savez, je le sais aussi, Je ne vous suis point inférieur.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Mais je veux parler au Tout-Puissant, Je veux plaider ma cause devant Dieu;
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Car vous, vous n’imaginez que des faussetés, Vous êtes tous des médecins de néant.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Que n’avez-vous gardé le silence? Vous auriez passé pour avoir de la sagesse.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Écoutez, je vous prie, ma défense, Et soyez attentifs à la réplique de mes lèvres.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Direz-vous en faveur de Dieu ce qui est injuste, Et pour le soutenir alléguerez-vous des faussetés?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Voulez-vous avoir égard à sa personne? Voulez-vous plaider pour Dieu?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
S’il vous sonde, vous approuvera-t-il? Ou le tromperez-vous comme on trompe un homme?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Certainement il vous condamnera, Si vous n’agissez en secret que par égard pour sa personne.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Sa majesté ne vous épouvantera-t-elle pas? Sa terreur ne tombera-t-elle pas sur vous?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Vos sentences sont des sentences de cendre, Vos retranchements sont des retranchements de boue.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Taisez-vous, laissez-moi, je veux parler! Il m’en arrivera ce qu’il pourra.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Pourquoi saisirais-je ma chair entre les dents? J’exposerai plutôt ma vie.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Voici, il me tuera; je n’ai rien à espérer; Mais devant lui je défendrai ma conduite.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Cela même peut servir à mon salut, Car un impie n’ose paraître en sa présence.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Écoutez, écoutez mes paroles, Prêtez l’oreille à ce que je vais dire.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Me voici prêt à plaider ma cause; Je sais que j’ai raison.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Quelqu’un disputera-t-il contre moi? Alors je me tais, et je veux mourir.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Seulement, accorde-moi deux choses Et je ne me cacherai pas loin de ta face:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Retire ta main de dessus moi, Et que tes terreurs ne me troublent plus.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Puis appelle, et je répondrai, Ou si je parle, réponds-moi!
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Quel est le nombre de mes iniquités et de mes péchés? Fais-moi connaître mes transgressions et mes péchés.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Pourquoi caches-tu ton visage, Et me prends-tu pour ton ennemi?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Veux-tu frapper une feuille agitée? Veux-tu poursuivre une paille desséchée?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
Pourquoi m’infliger d’amères souffrances, Me punir pour des fautes de jeunesse?
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Pourquoi mettre mes pieds dans les ceps, Surveiller tous mes mouvements, Tracer une limite à mes pas,
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Quand mon corps tombe en pourriture, Comme un vêtement que dévore la teigne?

< Ayubu 13 >