< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Voilà ce que mon œil a vu et ce qu'a entendu mon oreille.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Tout ce que vous savez je le sais, et, non plus que vous, je ne manque d'intelligence.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Je parlerai donc au Seigneur; je me plaindrai devant lui, s'il ne s'y oppose pas.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Vous êtes des médecins iniques, et il y a des remèdes pour tous les maux.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Que n'avez-vous gardé le silence? la sagesse vous viendrait.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Ecoutez les reproches de ma bouche; recueillez le jugement que prononcent mes lèvres.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
N'est-ce pas devant le Seigneur que vous avez discouru et que vous avez dit des mensonges?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Obéissez-vous à ses ordres? Non, vous vous étiez de vous-mêmes constitués juges.
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
C'est bien, s'il suit vos traces; et si, en tout ce que vous avez fait, vous vous êtes conformés à sa pensée,
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Il ne vous adressera pas le moindre blâme. Mais si, en secret, vous avez eu égard aux apparences,
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Est-ce que son tourbillon ne vous enlèvera pas? L'épouvante qu'il répand tombera sur vous.
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Votre orgueil se dispersera comme de la cendre; votre corps sera comme de la boue.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Ne m'interrompez pas; laissez-moi dire, et mon courroux se calmera.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Je prendrai, avec mes dents, ma chair, et je mettrai mon âme sur ma main.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Quand même le Tout-Puissant m'accablerait, puisque aussi bien il a commencé, je ne laisserais pas de parler et de me plaindre devant lui.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
C'est de là que viendra mon salut; car Dieu n'entendra de ma bouche aucune parole artificieuse.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Ecoutez, écoutez mes raisonnements, car je me dévoilerai à vous qui me prêtez l'oreille.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Me voici près du jugement, et je sens que je serai reconnu juste.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Car quel est celui qui comparaîtra avec moi devant le juge, pour que maintenant je me taise et que je déserte ma cause?
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Que deux choses mes soient accordées; alors, ô mon Dieu, je ne me cacherai point de vous.
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Détournez votre main qui me frappe; délivrez-moi de la crainte que vous inspirez.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Ensuite, appelez ma cause, et j'accourrai; accusez-moi, je ne vous ferai pas attendre ma défense.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Quels sont mes péchés et mes dérèglements? Apprenez-moi quels ils sont?
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
D'où vient que vous vous dérobez à mes regards? Montrez-moi le chemin qui mène à vous.
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Ne me considérez-vous pas comme un adversaire semblable à la feuille desséchée que le moindre souffle emporte, ou au brin d'herbe fanée qu'entraîne le vent?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
Et vous avez enregistré ce que je puis avoir fait de mal; et vous m'avez tenu compte des péchés de mon enfance.
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Vous avez mis mes pieds en des entraves; vous avez observé toutes mes œuvres; vous avez cherché l'empreinte de tous mes pas.
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Et je suis déjà comme une vieille outre, comme un manteau mangé des vers.