< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Voilà que mon œil a vu tout cela, mon oreille l’a entendu et compris.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Ce que vous savez, moi aussi je le sais, je ne vous suis en rien inférieur.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
Mais je veux parler au Tout-Puissant, je veux plaider ma cause avec Dieu.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
Car vous n’êtes que des charlatans, vous êtes tous des médecins inutiles.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Que ne gardiez-vous le silence! Il vous eût tenu lieu de sagesse.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Écoutez, je vous prie, ma défense, soyez attentifs au plaidoyer de mes lèvres.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Parlerez-vous mensonge en faveur de Dieu, pour lui, parlerez-vous tromperie?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Ferez-vous pour Dieu acception de personnes, vous constituerez-vous avocats?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Vous en saura-t-il gré, s’il sonde vos cœurs? Le tromperez-vous comme on trompe un homme?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Certainement il vous condamnera, si vous faites en secret acception de personnes.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Oui, sa majesté vous épouvantera, ses terreurs tomberont sur vous.
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Vos arguments sont des raisons de poussière, vos forteresses sont des forteresses d’argile.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Taisez-vous, laissez-moi, je veux parler; il m’en arrivera ce qu’il pourra.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Je veux prendre ma chair entre les dents, je veux mettre mon âme dans ma main.
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Quand il me tuerait, que je n’aurais rien à espérer, je défendrai devant lui ma conduite.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Mais il sera mon salut, car l’impie ne saurait paraître en sa présence.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Écoutez donc mes paroles, prêtez l’oreille à mon discours.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Voici que j’ai préparé ma cause, je sais que je serai justifié.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Est-il quelqu’un qui veuille plaider contre moi? À l’instant même je veux me taire et mourir.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Seulement épargne-moi deux choses, ô Dieu, et je ne me cacherai pas devant ta face:
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
éloigne ta main de dessus moi, et que tes terreurs ne m’épouvantent plus.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Après cela, appelle, et je répondrai; ou bien je parlerai d’abord, et tu me répondras.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Quel est le nombre de mes iniquités et de mes péchés? Fais-moi connaître mes transgressions et mes offenses.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Pourquoi cacher ainsi ton visage, et me regarder comme ton ennemi!
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Veux-tu donc effrayer une feuille agitée par le vent, poursuivre une paille desséchée,
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
pour que tu écrives contre moi des choses amères, pour que tu m’imputes les fautes de ma jeunesse,
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
pour que tu mettes mes pieds dans les ceps, que tu observes toutes mes démarches, que tu traces une limite à la plante de mes pieds,
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
alors que mon corps se consume comme un bois vermoulu, comme un vêtement que dévore la teigne.