< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
look! all to see: see eye my to hear: hear ear my and to understand to/for her
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
like/as knowledge your to know also I not to fall: fall I from you
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
but I to(wards) Almighty to speak: speak and to rebuke to(wards) God to delight in
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
and but you(m. p.) to smear deception to heal idol all your
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
who? to give: give be quiet be quiet [emph?] and to be to/for you to/for wisdom
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
to hear: hear please argument my and strife lips my to listen
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
to/for God to speak: speak injustice and to/for him to speak: speak deceit
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
face: kindness his to lift: kindness [emph?] if: surely no to/for God to contend [emph?]
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
pleasant for to search [obj] you if: surely no like/as to deceive in/on/with human to deceive in/on/with him
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
to rebuke to rebuke [obj] you if in/on/with secrecy face to lift: kindness [emph?]
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
not elevation his to terrify [obj] you and dread his to fall: fall upon you
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
memorial your proverb ashes to/for back/rim/brow clay back/rim/brow your
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
be quiet from me and to speak: speak I and to pass upon me what?
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
upon what? to lift: raise flesh my in/on/with tooth my and soul: life my to set: put in/on/with palm my
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
look! to slay me (to/for him *Q(K)*) to wait: hope surely way: conduct my to(wards) face his to rebuke
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
also he/she/it to/for me to/for salvation for not to/for face: before his profane to come (in): come
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
to hear: hear to hear: hear speech my and declaration my in/on/with ear your
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
behold please to arrange justice: judgement to know for I to justify
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
who? he/she/it to contend with me me for now be quiet and to die
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
surely two not to make: offer with me me then from face your not to hide
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
palm your from upon me to remove and terror your not to terrify me
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
and to call: call to and I to answer or to speak: speak and to return: reply me
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
like/as what? to/for me iniquity: crime and sin transgression my and sin my to know me
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
to/for what? face your to hide and to devise: think me to/for enemy to/for you
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
leaf to drive to tremble and [obj] stubble dry to pursue
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
for to write upon me gall and to possess: possess me iniquity: crime youth my
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
and to set: put in/on/with stock foot my and to keep: look at all way my upon root foot my to engrave
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
and he/she/it like/as rottenness to become old like/as garment to eat him moth