< Ayubu 13 >

1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Lo! all [this], hath mine own eye seen, —Mine ear hath heard and understood it:
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
Just as ye know, I too, know, I, fall not short, of you.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
But indeed, I, unto the Almighty, would speak, and, to direct my argument unto GOD, would I be well pleased.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
For, in truth, ye, do besmear with falsehood, Worthless physicians, all of you!
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Oh that ye would, altogether hold your peace, and it should serve you for wisdom!
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Hear, I pray you, the argument of my mouth, and, to the pleadings of my lips, give heed: —
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Is it, for God, ye would speak perversely? And, for him, would ye speak deceit:
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Even, for him, would ye be partial? Or, for GOD, would ye [so] plead?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Would it be well, when he searched you out? Or, as one might jest with a mortal, would ye jest, with him?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
He will, severely rebuke, you, if ye are secretly partial.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Shall not, his majesty, overwhelm you? and, the dread of him, fall upon you?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Are not your memorable sayings, proverbs of ashes? Breastworks of clay, your breastworks?
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Quietly let me alone, that, I, may speak out, then let come on me, what may.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
In any case, I will take up my flesh in my teeth, and, my life, will I put in my hand:
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Lo! he may slay me, [yet], for him, will I wait, —Nevertheless, my ways—unto his face, will I show to be right:
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
Even he, will be on my side—unto salvation, For, not before his face, shall any impious person come.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Hear ye patiently my speech, and be my declaration in your ears.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Lo! I pray you, I have set forth in order a plea, I know that, I, shall be found right.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Who is it that shall contend with me? For, now, if I should hold my peace, why! I should breathe my last!
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Only, two things, do thou not with me, then, from thy face, will I not hide me: —
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Thy hand—from off me, take thou far away, and, thy terror, let it not startle me!
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Then call thou, and, I, will answer, Or I will speak, and reply thou unto me.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
How many are mine iniquities and sins? My transgression and my sin, let me know!
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Wherefore, thy face, shouldst thou hide? Or count me, as an enemy to thee?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
A driven leaf, wilt thou cause to tremble? Or, dry stubble, wilt thou pursue?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
For thou writest, against me, bitter things, and dost make me inherit the iniquities of my youth;
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
And thou dost put—in the stocks—my feet, and observest all my paths, Against the roots of my feet, thou dost cut out a bound;
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
And, a man himself, as a rotten thing, weareth out, as a garment which the moth hath eaten.

< Ayubu 13 >