< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Lo! all this mine eye hath seen; Mine ear hath heard and understood it.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
What ye know, I know also; I am not inferior to you.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
But O that I might speak with the Almighty! O that I might reason with God!
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
For ye are forgers of lies; Physicians of no value, all of you!
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
O that ye would altogether hold your peace! This, truly, would be wisdom in you.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Hear, I pray you, my arguments; Attend to the pleadings of my lips!
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Will ye speak falsehood for God? Will ye utter deceit for him?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Will ye be partial to his person? Will ye contend earnestly for God?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Will it be well for you, if he search you thoroughly? Can ye deceive him, as one may deceive a man?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
Surely he will rebuke you, If ye secretly have respect to persons.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Doth not his majesty make you afraid, And his dread fall upon you?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Your maxims are words of dust; Your fortresses are fortresses of clay.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Hold your peace, and let me speak: And then come upon me what will!
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Why do I take my flesh in my teeth, And put my life in my hand?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Lo! he slayeth me, and I have no hope! Yet will I justify my ways before him.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
This also shall be my deliverance; For no unrighteous man will come before him.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Hear attentively my words, And give ear to my declaration!
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Behold, I have now set in order my cause; I know that I am innocent.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Who is he that can contend with me? For then would I hold my peace, and die!
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Only do not unto me two things, Then will I not hide myself from thy presence;
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Let not thy hand be heavy upon me, And let not thy terrors make me afraid:
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Then call upon me, and I will answer; Or I will speak, and answer thou me.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
How many are my iniquities and sins? Make me to know my faults and transgressions.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Wherefore dost thou hide thy face, And account me as thine enemy?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Wilt thou put in fear the driven leaf? Wilt thou pursue the dry stubble?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
For thou writest bitter things against me, And makest me inherit the sins of my youth.
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Yea, thou puttest my feet in the stocks, And waterest all my paths; Thou hemmest in the soles of my feet.
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
And I, like an abandoned thing, shall waste away; Like a garment which is moth-eaten.