< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Loe, mine eye hath seene all this: mine eare hath heard, and vnderstande it.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
I knowe also as much as you knowe: I am not inferiour vnto you.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
But I will speake to the Almightie, and I desire to dispute with God.
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
For in deede ye forge lyes, and all you are physitions of no value.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Oh, that you woulde holde your tongue, that it might be imputed to you for wisedome!
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Nowe heare my disputation, and giue eare to the arguments of my lips.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Will ye speake wickedly for Gods defence, and talke deceitfully for his cause?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Will ye accept his person? or will ye contende for God?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Is it well that he shoulde seeke of you? will you make a lye for him, as one lyeth for a man?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
He will surely reprooue you, if ye doe secretly accept any person.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Shall not his excellencie make you afraid? and his feare fall vpon you?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Your memories may be compared vnto ashes, and your bodyes to bodyes of clay.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Holde your tongues in my presence, that I may speake, and let come vpon what will.
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Wherefore doe I take my flesh in my teeth, and put my soule in mine hande?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Loe, though he slay me, yet will I trust in him, and I will reprooue my wayes in his sight.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
He shalbe my saluation also: for the hypocrite shall not come before him.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Heare diligently my wordes, and marke my talke.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Beholde nowe: if I prepare me to iudgement, I knowe that I shalbe iustified.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Who is he, that will pleade with me? for if I nowe holde my tongue, I dye.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
But doe not these two things vnto me: then will I not hide my selfe from thee.
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Withdrawe thine hande from me, and let not thy feare make me afraide.
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Then call thou, and I will answere: or let me speake, and answere thou me.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
Howe many are mine iniquities and sinnes? shewe me my rebellion, and my sinne.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Wherefore hidest thou thy face, and takest me for thine enemie?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Wilt thou breake a leafe driuen to and from? and wilt thou pursue the drie stubble?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
For thou writest bitter things against me, and makest me to possesse the iniquities of my youth.
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
Thou puttest my feete also in the stocks, and lookest narrowly vnto all my pathes, and makest the print thereof in ye heeles of my feet.
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
Such one consumeth like a rotten thing, and as a garment that is motheaten.