< Ayubu 13 >
1 “Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
Lo, mine eye hath seen all [this], mine ear hath heard and understood it.
2 Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
What ye know, I know also: I am not inferior to you.
3 Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
But I will speak to the Almighty, and will find pleasure in reasoning with God;
4 Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
For ye indeed are forgers of lies, ye are all physicians of no value.
5 Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
Oh that ye would be altogether silent! and it would be your wisdom.
6 Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
Hear now my defence, and hearken to the pleadings of my lips.
7 Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
Will ye speak unrighteously for God? and for him speak deceit?
8 Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
Will ye accept his person? will ye contend for God?
9 Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
Will it be well if he should search you out? or as one mocketh at a man, will ye mock at him?
10 Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
He will certainly reprove you, if ye do secretly accept persons.
11 Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Shall not his excellency terrify you? and his dread fall upon you?
12 Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
Your memorable sayings are proverbs of ashes, your bulwarks are bulwarks of mire.
13 “Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
Hold your peace from me, and I will speak, and let come on me what [will]!
14 Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
Wherefore should I take my flesh in my teeth, and put my life in my hand?
15 Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
Behold, if he slay me, yet would I trust in him; but I will defend mine own ways before him.
16 Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
This also shall be my salvation, that a profane man shall not come before his face.
17 Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
Hear attentively my speech and my declaration with your ears.
18 Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
Behold now, I have ordered the cause; I know that I shall be justified.
19 Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Who is he that contendeth with me? For if I were silent now, I should expire.
20 “Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
Only do not two things unto me; then will I not hide myself from thee.
21 Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
Withdraw thy hand far from me; and let not thy terror make me afraid:
22 Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
Then call, and I will answer; or I will speak, and answer thou me.
23 Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
How many are mine iniquities and sins? Make me to know my transgression and my sin.
24 Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
Wherefore dost thou hide thy face, and countest me for thine enemy?
25 Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
Wilt thou terrify a driven leaf? and wilt thou pursue dry stubble?
26 Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
For thou writest bitter things against me, and makest me to possess the iniquities of my youth;
27 Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
And thou puttest my feet in the stocks, and markest all my paths; thou settest a bound about the soles of my feet; —
28 “Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.
One who, as a rotten thing consumeth, as a garment that the moth eateth.