< Ayubu 12 >
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
“Kendinizi bir şey sandığınız belli, Ama bilgelik de sizinle birlikte ölecek!
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
Sizin kadar benim de aklım var, Sizden aşağı kalmam. Kim bilmez bunları?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
“Gülünç oldum dostlarıma, Ben ki, Tanrı'ya yakarırdım, yanıtlardı beni. Doğru ve kusursuz adam gülünç oldu.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
Kaygısızlar felaketi küçümser, Ayağı kayanı umursamaz.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
Soyguncuların çadırlarında rahatlık var, Tanrı'yı gazaba getirenler güvenlik içinde, Tanrı'ya değil, kendi bileklerine güveniyorlar.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
“Ama şimdi sor hayvanlara, sana öğretsinler, Gökte uçan kuşlara sor, sana anlatsınlar,
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Toprağa söyle, sana öğretsin, Denizdeki balıklara sor, sana bilgi versinler.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Hangisi bilmez Bunu RAB'bin yaptığını?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
Her yaratığın canı, Bütün insanlığın soluğu O'nun elindedir.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Damağın yemeği tattığı gibi Kulak da sözleri denemez mi?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Bilgelik yaşlılarda, Akıl uzun yaşamdadır.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
“Bilgelik ve güç Tanrı'ya özgüdür, O'ndadır öğüt ve akıl.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
O'nun yıktığı onarılamaz, O'nun hapsettiği kişi özgür olamaz.
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
Suları tutarsa, kuraklık olur, Salıverirse dünyayı sel götürür.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
Güç ve zafer O'na aittir, Aldanan da aldatan da O'nundur.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
Danışmanları çaresiz kılar, Yargıçları çıldırtır.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
Kralların bağladığı bağı çözer, Bellerine kuşak bağlar.
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
Kâhinleri çaresiz kılar, Koltuklarında yıllananları devirir.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
Güvenilir danışmanları susturur, Yaşlıların aklını alır.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
Rezalet saçar soylular üzerine, Güçlülerin kuşağını gevşetir.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
Karanlıkların derin sırlarını açar, Ölüm gölgesini aydınlığa çıkarır.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
Ulusları büyütür, ulusları yok eder, Ulusları genişletir, ulusları sürgün eder.
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
Dünya önderlerinin aklını başından alır, Yolu izi belirsiz bir çölde dolaştırır onları.
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
Karanlıkta el yordamıyla yürür, ışık yüzü görmezler; Sarhoş gibi dolaştırır onları.