< Ayubu 12 >
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
Ciertamente que vosotros sois el pueblo; y con vosotros morirá la sabiduría.
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
También tengo yo seso como vosotros; no soy yo menos que vosotros: ¿y quién habrá que no pueda decir otro tanto?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
Yo soy uno de quien su amigo se mofa, que invoca á Dios, y él le responde: con todo, el justo y perfecto es escarnecido.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
Aquel cuyos pies van á resbalar, [es como] una lámpara despreciada de aquel que está á sus anchuras.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
Prosperan las tiendas de los ladrones, y los que provocan á Dios viven seguros; en cuyas manos él ha puesto [cuanto tienen].
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
Y en efecto, pregunta ahora á las bestias, que ellas te enseñarán; y á las aves de los cielos, que ellas te lo mostrarán:
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
O habla á la tierra, que ella te enseñará; los peces de la mar te [lo] declararán también.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
¿Qué cosa de todas estas no entiende que la mano de Jehová la hizo?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
En su mano está el alma de todo viviente, y el espíritu de toda carne humana.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Ciertamente el oído distingue las palabras, y el paladar gusta las viandas.
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
En los viejos está la ciencia, y en la larga edad la inteligencia.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
Con Dios está la sabiduría y la fortaleza; suyo es el consejo y la inteligencia.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
He aquí, él derribará, y no será edificado: encerrará al hombre, y no habrá quien le abra.
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
He aquí, él detendrá las aguas, y se secarán; él las enviará, y destruirán la tierra.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
Con él está la fortaleza y la existencia; suyo es el que yerra, y el que hace errar.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
El hace andar á los consejeros desnudos [de consejo], y hace enloquecer á los jueces.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
El suelta la atadura de los tiranos, y ata el cinto á sus lomos.
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
El lleva despojados á los príncipes, y trastorna á los poderosos.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
El impide el labio á los que dicen verdad, y quita á los ancianos el consejo.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
El derrama menosprecio sobre los príncipes, y enflaquece la fuerza de los esforzados.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
El descubre las profundidades de las tinieblas, y saca á luz la sombra de muerte.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
El multiplica las gentes, y él las destruye: él esparce las gentes, y las torna á recoger.
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
El quita el seso de las cabezas del pueblo de la tierra, y háceles que se pierdan vagueando sin camino:
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
Van á tientas como en tinieblas y sin luz, y los hace errar como borrachos.