< Ayubu 12 >
Então Job respondeu, e disse:
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
Na verdade, que só vós sois o povo, e convosco morrerá a sabedoria.
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
Também eu tenho um coração como vós, e não vos sou inferior: e quem não sabe tais coisas como estas?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
Eu sou irrisão aos meus amigos; eu, que invoco a Deus, e ele me responde; o justo e o reto servem de irrisão.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
Tocha desprezível é na opinião do que está descançado, aquele que está pronto a tropeçar com os pés.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
As tendas dos assoladores tem descanço, e os que provocam a Deus estão seguros; nas suas mãos Deus lhes põe tudo.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
Mas, pergunta agora às bestas, e cada uma delas to ensinará: e às aves dos céus, e elas to farão saber;
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Ou fala com a terra, e ela to ensinará: até os peixes do mar to contarão.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Quem não entende por todas estas coisas que a mão do Senhor faz isto?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
Em cuja mão está a alma de tudo quanto vive, e o espírito de toda a carne humana.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Porventura o ouvido não provará as palavras, como o paladar gosta as comidas?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Com os idosos está a sabedoria, e na longura de dias o entendimento.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
Com ele está a sabedoria e a força: conselho e entendimento tem.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
Eis que ele derriba, e não se reedificará: encerra o homem, e não se lhe abrirá.
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
Eis que ele retém as águas, e se secam; e as larga, e transtornam a terra.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
Com ele está a força e a sabedoria: seu é o errante e o que o faz errar.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
Aos conselheiros leva despojados, e aos juízes faz desvairar.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
Solta a atadura dos reis, e ata o cinto aos seus lombos.
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
Aos príncipes leva despojados, aos poderosos transtorna.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
Aos acreditados tira a fala, e toma o entendimento aos velhos.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
Derrama desprezo sobre os príncipes, e afrouxa o cinto dos violentos.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
As profundezas das trevas manifesta, e a sombra da morte traz à luz.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
Multiplica as gentes e as faz perecer; espalha as gentes, e as guia.
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
Tira o coração aos chefes das gentes da terra, e os faz vaguear pelos desertos, sem caminho.
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
Nas trevas andam às apalpadelas, sem terem luz, e os faz desatinar como ébrios.