< Ayubu 12 >
Then Job said [to his three friends],
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
“You (talk as though/You think) [SAR] that you are the people [whom everyone should listen to], and that when you die, there will be no more wise people.
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
But I have as much good sense as you do; I am (not less wise than/certainly as wise as [LIT]) you. Certainly everyone knows [RHQ] all that you have said.
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
My friends all laugh at me now. Previously I habitually requested God to help me, and he answered/helped me. I am righteous, a very godly man [DOU], but everyone laughs at me.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
Those [like you] who have no troubles make fun of me; they cause those [like me] who are already suffering to have more troubles.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
Bandits live peacefully, and no one threatens those who cause God to become angry; their own strength is the god [that they worship].
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
“But ask the wild animals [what they know about God], and [if they could speak] they would teach you. [If you could] ask the birds, they would tell you.
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
[If you could] ask the creatures [that crawl] on the ground, or the fish in the sea, they would tell you [about God].
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
All of them certainly know [RHQ] that it is Yahweh who has made them with his hands.
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
He directs the lives of all living creatures; he gives breath to all [us] humans [to enable us to remain alive].
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
And when we [SYN] hear what other people [like you] say, we [RHQ] think carefully about what they say [to determine what is good and what is bad], like we [SYN] taste food [to determine what is good and what is bad].
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Old people are [often] very wise, and because of having lived many years, they understand much,
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
but God is wise and very powerful; he has good sense and understands [everything].
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
If he tears [something] down, no one can rebuild it; if he puts someone in prison, no one can open [the prison doors to allow that person to escape].
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
When he prevents rain from falling, everything dries up. When he causes a lot of rain to fall, [the result is that] there are floods.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
He is the one who is truly strong and wise; he rules over those who deceive others and those whom they deceive.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
He [sometimes] causes [the king’s] officials to no longer be wise, and he causes judges to become foolish.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
He takes from kings the robes that they wear and puts loincloths around their waists, [causing them to become slaves].
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
He takes from priests the sacred clothes that they wear, [with the result that they no longer can do their work], and takes power from those who rule others.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
He [sometimes] causes those whom others trust to be unable to speak, and he causes old men to no longer have good sense.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
He causes those who have authority to be despised, and he causes those who are powerful to no longer have any power/strength.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
He causes things that are hidden in the darkness to be revealed.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
He causes some nations to become very great, and [later] he destroys them; he causes the territory of some nations to become much larger, and [later] he causes them to be defeated and their people to be scattered.
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
He causes [some] rulers to become foolish/stupid, and then he causes them to wander around, lost, in an barren desert.
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
They grope around in the darkness, without any light, and he causes them to stagger like [SIM] people who are drunk.”