< Ayubu 12 >
And Job answered and said,
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
So then you [alone] are men, and wisdom shall die with you?
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
[But] I also have a heart as well as you.
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
For a righteous and blameless man has become a subject for mockery.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
For it had been ordained that he should fall under others at the appointed time, and that his houses should be spoiled by transgressors: let not however any one trust that, being evil, he shall be [held] guiltless,
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
even as many as provoke the Lord, as if there were indeed to be no inquisition [made] of them.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
But ask now the beasts, if they may speak to you; and the birds of the air, if they may declare to you.
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Tell the earth, if it may speak to you: and the fishes of the sea shall explain to you.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Who then has not known in all these things, that the hand of the Lord has made them?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
Whereas the life of all living things is in his hand, and the breath of every man.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
For the ear tries words, and the palate tastes meats.
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
In length of time is wisdom, and in long life knowledge.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
With him are wisdom and power, with him counsel and understanding.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
If he should cast down, who will build up? if he should shut up against man, who shall open?
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
If he should withhold the water, he will dry the earth: and if he should let it loose, he overthrows and destroys it.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
With him are strength and power: he has knowledge and understanding.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
He leads counselors away captive, and maddens the judges of the earth.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
He seats kings upon thrones, and girds their loins with a girdle.
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
He sends away priests into captivity, and overthrows the mighty ones of the earth.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
He changes the lips of the trusty, and he knows the understanding of the elders.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
He pours dishonor upon princes, and heals the lowly.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
Revealing deep things out of darkness: and he has brought into light the shadow of death.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
Causing the nations to wander, and destroying them: overthrowing the nations, and leading them [away].
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
Perplexing the minds of the princes of the earth: and he causes them to wander in a way, they have not known, [saying],
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
Let them grope [in] darkness, and [let there be] no light, and let them wander as a drunken man.