< Ayubu 12 >
And Job answered and said,
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
Truly ye are the people, and wisdom shall die with you!
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
I also have understanding as well as you; I am not inferior to you; and who knoweth not such things as these?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
I am to be one that is a derision to his friend, I who call upon God, and whom he will answer: a derision is the just upright [man].
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
He that is ready to stumble with the foot is a lamp despised in the thought of him that is at ease.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
The tents of desolators are in peace, and they that provoke God are secure; into whose hand God bringeth.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
But ask now the beasts, and they shall teach thee; and the fowl of the heavens, and they shall tell thee;
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Or speak to the earth, and it shall teach thee; and the fishes of the sea shall declare unto thee.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Who knoweth not in all these, that the hand of Jehovah hath wrought this?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
In whose hand is the soul of every living thing, and the spirit of all flesh of man.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Doth not the ear try words, as the palate tasteth food?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
With the aged is wisdom, and in length of days understanding.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
With him is wisdom and might; he hath counsel and understanding.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
Behold, he breaketh down, and it is not built again; he shutteth up a man, and there is no opening.
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
Behold, he withholdeth the waters, and they dry up; and he sendeth them out, and they overturn the earth.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
With him is strength and effectual knowledge; the deceived and the deceiver are his.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
He leadeth counsellors away spoiled, and judges maketh he fools;
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
He weakeneth the government of kings, and bindeth their loins with a fetter;
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
He leadeth priests away spoiled, and overthroweth the mighty;
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
He depriveth of speech the trusty, and taketh away the judgment of the elders;
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
He poureth contempt upon nobles, and slackeneth the girdle of the mighty;
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
He discovereth deep things out of darkness, and bringeth out into light the shadow of death;
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
He increaseth the nations, and destroyeth them; he spreadeth out the nations, and bringeth them in;
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
He taketh away the understanding of the chiefs of the people of the earth, and causeth them to wander in a pathless waste.
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
They grope in the dark without light, and he maketh them to stagger like a drunkard.