< Ayubu 12 >
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
“Truly then you are the people with whom wisdom itself will die!
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
But I also have a mind; I am not inferior to you. Who does not know such things as these?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
I am a laughingstock to my friends, though I called on God, and He answered. The righteous and upright man is a laughingstock.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
The one at ease scorns misfortune as the fate of those whose feet are slipping.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
The tents of robbers are safe, and those who provoke God are secure— those who carry their god in their hands.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
But ask the animals, and they will instruct you; ask the birds of the air, and they will tell you.
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
Or speak to the earth, and it will teach you; let the fish of the sea inform you.
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Which of all these does not know that the hand of the LORD has done this?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
The life of every living thing is in His hand, as well as the breath of all mankind.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Does not the ear test words as the tongue tastes its food?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Wisdom is found with the elderly, and understanding comes with long life.
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
Wisdom and strength belong to God; counsel and understanding are His.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
What He tears down cannot be rebuilt; the man He imprisons cannot be released.
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
If He holds back the waters, they dry up, and if He releases them, they overwhelm the land.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
True wisdom and power belong to Him. The deceived and the deceiver are His.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
He leads counselors away barefoot and makes fools of judges.
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
He loosens the bonds placed by kings and fastens a belt around their waists.
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
He leads priests away barefoot and overthrows the established.
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
He deprives the trusted of speech and takes away the discernment of elders.
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
He pours out contempt on nobles and disarms the mighty.
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
He reveals the deep things of darkness and brings deep shadows into light.
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
He makes nations great and destroys them; He enlarges nations, then disperses them.
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
He deprives the earth’s leaders of reason and makes them wander in a trackless wasteland.
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
They grope in the darkness without light; He makes them stagger like drunkards.