< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
Saa tog Job til Orde og svarede:
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
Ja, sandelig, I er de rette, med eder dør Visdommen ud!
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
Ogsaa jeg har som I Forstand, staar ikke tilbage for eder, hvo kender vel ikke sligt?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
Til Latter for Venner er den, der raabte til Gud og fik Svar, den retfærdige er til Latter.
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
I Ulykke falder de fromme, den sorgløse spotter Faren, hans Fod staar fast, mens Fristen varer.
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
I Fred er Voldsmænds Telte, og trygge er de, der vækker Guds Vrede, den, der fører Gud i sin Haand.
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
Spørg dog Kvæget, det skal lære dig, Himlens Fugle, de skal oplyse dig,
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
se til Jorden, den skal lære dig lad Havets Fisk fortælle dig det!
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
Hvem blandt dem alle ved vel ikke, at HERRENS Haand har skabt det;
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
han holder alt levendes Sjæl i sin Haand, alt Menneskekødets Aand!
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
Prøver ej Øret Ord, og smager ej Ganen Maden?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
Er Alderdom eet med Visdom, Dagenes Række med Indsigt?
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
Hos ham er der Visdom og Vælde, hos ham er der Raad og Indsigt.
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
Hvad han river ned, det bygges ej op, den, han lukker inde, kommer ej ud;
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
han dæmmer for Vandet, og Tørke kommer, han slipper det løs, og det omvælter Jorden.
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
Hos ham er der Kraft og Fasthed; den, der farer og fører vild, er hans Værk.
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
Raadsherrer fører han nøgne bort, og Dommere gør han til Taaber;
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
han løser, hvad Konger bandt, og binder dem Reb om Lænd;
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
Præster fører han nøgne bort og styrter ældgamle Slægter;
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
han røver de dygtige Mælet og tager de gamles Sans;
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
han udøser Haan over Fyrster og løser de stærkes Bælte;
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
han drager det skjulte frem af Mørket og bringer Mulmet for Lyset,
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
gør Folkene store og lægger dem øde, udvider Folkeslags Grænser og fører dem atter bort;
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
han tager Jordens Høvdingers Vid og lader dem rave i vejløst Øde;
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
de famler i Mørke uden Lys og raver omkring som drukne.

< Ayubu 12 >