< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
的確,只有你們是有知識的子民;那麼,你們一死,智慧也與你們一同喪亡!
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
其實,我和你們有同樣的心理,我並不亞於你們! 誰不知道這些事﹖
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
我這呼籲天主而蒙應允的人,卻被他的友人所嘲笑,無辜的義人卻成了笑柄。
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
幸運的人心想:遭難的人應受蔑視,失足的人應再予以打擊。
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
但是,強盜的帳幕竟能安全,觸怒天主的人,以勢力為神的人卻享平安。
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
請你詢問走獸,牠們也會開導你;詢問天上的飛鳥,牠們也會告訴你;
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
地上的爬蟲也會教訓你,海中的魚族也會給你說明。
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
牠們中有誰不知道:是天主的手創造了這一切﹖
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
因為一切活物的生魂,一切血肉之人的靈魂,都握在他手中。
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
耳朵不是為明辨言語,口腔不是為辨嘗食物嗎﹖
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
白髮老人是有智慧的,年紀大者是有見識的;
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
但智慧和能力同在天主內,智慧與見識是天主所有。
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
他若拆毀,人不能再建;他若拘禁,人不得開釋。
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
他若制水,水便乾涸;他若放水,水便沖毀大地。
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
力量與才能,為他所有;受騙者與騙人者,都屬於他。
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
他使謀士糊塗,使判官愚蠢;
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
他解除君王所繫的玉帶,將繩索捆在他們的腰間;
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
他使司祭赤足而行,推倒掌握大權者;
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
奪去忠貞者的辯才,剝去年老者的理智:
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
使貴人備受侮辱,使勇士的腰帶鬆弛;
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
使隱秘的事由暗處彰顯,使黑暗進入光明;
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
使邦國興起而又滅亡,使民族強大而又消散;
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
剝去國君的理智,使他們漂泊於無路的荒野中,
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
在無光的黑暗中摸索,踉蹌猶如醉漢。

< Ayubu 12 >