< Ayubu 10 >

1 “Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
ESTÁ mi alma aburrida de mi vida: daré yo suelta á mi queja sobre mí, hablaré con amargura de mi alma.
2 Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
Diré á Dios: no me condenes; hazme entender por qué pleiteas conmigo.
3 Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
¿Parécete bien que oprimas, que deseches la obra de tus manos, y que resplandezcas sobre el consejo de los impíos?
4 Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
¿Tienes tú ojos de carne? ¿ves tú como ve el hombre?
5 Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
¿Son tus días como los días del hombre, ó tus años como los tiempos humanos,
6 ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
Para que inquieras mi iniquidad, y busques mi pecado,
7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
Sobre saber tú que no soy impío, y que no hay quien de tu mano libre?
8 “Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
Tus manos me formaron y me compusieron todo en contorno: ¿y así me deshaces?
9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Acuérdate ahora que como á lodo me diste forma: ¿y en polvo me has de tornar?
10 Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
¿No me fundiste como leche, y como un queso me cuajaste?
11 ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
Vestísteme de piel y carne, y cubrísteme de huesos y nervios.
12 Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
Vida y misericordia me concediste, y tu visitación guardó mi espíritu.
13 “Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
Y estas cosas tienes guardadas en tu corazón; yo sé que esto está cerca de ti.
14 Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
Si pequé, tú me has observado, y no me limpias de mi iniquidad.
15 Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
Si fuere malo, ¡ay de mí! y si fuere justo, no levantaré mi cabeza, estando harto de deshonra, y de verme afligido.
16 Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
Y subirá de punto, [pues] me cazas como á león, y tornas á hacer en mí maravillas.
17 Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
Renuevas contra mí tus plagas, y aumentas conmigo tu furor, remudándose sobre mí ejércitos.
18 “Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
¿Por qué me sacaste de la matriz? Habría yo espirado, y no me vieran ojos.
19 Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
Fuera, como si nunca hubiera sido, llevado desde el vientre á la sepultura.
20 Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
¿No son mis días poca cosa? Cesa pues, y déjame, para que me conforte un poco.
21 kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
Antes que vaya para no volver, á la tierra de tinieblas y de sombra de muerte;
22 nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”
Tierra de oscuridad, lóbrega como sombra de muerte, sin orden, y que aparece como [la] oscuridad [misma].

< Ayubu 10 >