< Ayubu 10 >

1 “Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
A minha alma tem tedio á minha vida: darei livre curso á minha queixa, fallarei na amargura da minha alma.
2 Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
Direi a Deus: Não me condemnes: faze-me saber porque contendes comigo.
3 Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
Parece-te bem que me opprimas? que rejeites o trabalho das tuas mãos? e resplandeças sobre o conselho dos impios?
4 Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
Tens tu porventura olhos de carne? vês tu como vê o homem?
5 Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
São os teus dias como os dias do homem? Ou são os teus annos como os annos de um homem,
6 ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
Para te informares da minha iniquidade, e averiguares o meu peccado?
7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
Bem sabes tu que eu não sou impio: todavia ninguem ha que me livre da tua mão.
8 “Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
As tuas mãos me fizeram e me formaram todo em roda; comtudo me consomes.
9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Peço-te que te lembres de que como barro me formaste e me farás tornar em pó.
10 Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
Porventura não me vasaste como leite, e como queijo me não coalhaste?
11 ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
De pelle e carne me vestiste, e com ossos e nervos me ligaste.
12 Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
Vida e beneficencia me fizeste: e o teu cuidado guardou o meu espirito.
13 “Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
Porém estas coisas as occultaste no teu coração: bem sei eu que isto esteve comtigo.
14 Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
Se eu peccar, tu me observas; e da minha iniquidade não me escusarás.
15 Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
Se fôr impio, ai de mim! e se fôr justo, não levantarei a minha cabeça: farto estou de affronta; e olho para a minha miseria.
16 Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
Porque se vae crescendo; tu me caças como a um leão feroz: tornas-te, e fazes maravilhas contra mim.
17 Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
Tu renovas contra mim as tuas testemunhas, e multiplicas contra mim a tua ira; revezes e combate estão comigo.
18 “Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
Por quepois me tiraste da madre? Ah se então dera o espirito, e olhos nenhuns me vissem!
19 Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
Que tivera sido como se nunca fôra: e desde o ventre fôra levado á sepultura!
20 Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
Porventura não são poucos os meus dias? cessa pois, e deixa-me, para que por um pouco eu tome alento;
21 kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
Antes que vá e d'onde nunca torne, á terra da escuridão e da sombra da morte;
22 nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”
Terra escurissima, como a mesma escuridão, terra da sombra, da morte e sem ordem alguma e onde a luz é como a escuridão.

< Ayubu 10 >