< Ayubu 10 >

1 “Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
“My soul is weary of my life. I will give free course to my complaint. I will speak in the bitterness of my soul.
2 Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
I will tell God, ‘Do not condemn me. Show me why you contend with me.
3 Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
Is it good to you that you should oppress, that you should despise the work of your hands, and smile on the counsel of the wicked?
4 Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
Do you have eyes of flesh? Or do you see as man sees?
5 Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
Are your days as the days of mortals, or your years as man’s years,
6 ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
that you inquire after my iniquity, and search after my sin?
7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
Although you know that I am not wicked, there is no one who can deliver out of your hand.
8 “Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
“‘Your hands have framed me and fashioned me altogether, yet you destroy me.
9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Remember, I beg you, that you have fashioned me as clay. Will you bring me into dust again?
10 Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
Have not you poured me out like milk, and curdled me like cheese?
11 ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
You have clothed me with skin and flesh, and knit me together with bones and sinews.
12 Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
You have granted me life and loving kindness. Your visitation has preserved my spirit.
13 “Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
Yet you hid these things in your heart. I know that this is with you:
14 Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
if I sin, then you mark me. You will not acquit me from my iniquity.
15 Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
If I am wicked, woe to me. If I am righteous, I still will not lift up my head, being filled with disgrace, and conscious of my affliction.
16 Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
If my head is held high, you hunt me like a lion. Again you show yourself powerful to me.
17 Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
You renew your witnesses against me, and increase your indignation on me. Changes and warfare are with me.
18 “Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
“‘Why, then, have you brought me out of the womb? I wish I had given up the spirit, and no eye had seen me.
19 Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
I should have been as though I had not been. I should have been carried from the womb to the grave.
20 Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
Are not my days few? Stop! Leave me alone, that I may find a little comfort,
21 kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
before I go where I will not return from, to the land of darkness and of the shadow of death;
22 nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”
the land dark as midnight, of the shadow of death, without any order, where the light is as midnight.’”

< Ayubu 10 >