< Ayubu 10 >

1 “Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
Min Sjæl er led ved mit Liv, frit Løb vil jeg give min Klage over ham, i min bitre Sjælenød vil jeg tale,
2 Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
sige til Gud: Fordøm mig dog ikke, lad mig vide, hvorfor du tvister med mig!
3 Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
Gavner det dig at øve Vold, at forkaste det Værk, dine Hænder danned, men smile til gudløses Raad?
4 Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
Har du da Kødets Øjne, ser du, som Mennesker ser,
5 Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
er dine Dage som Menneskets Dage, er dine Aar som Mandens Dage,
6 ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
siden du søger efter min Brøde, leder efter min Synd,
7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
endskønt du ved, jeg ikke er skyldig; men af din Haand er der ingen Redning!
8 “Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
Dine Hænder gjorde og danned mig først, saa skifter du Sind og gør mig til intet!
9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
Kom i Hu, at du dannede mig som Ler, og til Støv vil du atter gøre mig!
10 Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
Mon du ikke hældte mig ud som Mælk og lod mig skørne som Ost,
11 ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
iklædte mig Hud og Kød og fletted mig sammen med Ben og Sener?
12 Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
Du gav mig Liv og Livskraft, din Omhu vogted min Aand —
13 “Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
og saa gemte du dog i dit Hjerte paa dette, jeg skønner, dit Øjemed var:
14 Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
Synded jeg, vogted du paa mig og tilgav ikke min Brøde.
15 Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
I Fald jeg forbrød mig, da ve mig! Var jeg retfærdig, jeg skulde dog ikke løfte mit Hoved, men mættes med Skændsel, kvæges med Nød.
16 Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
Knejsed jeg, jog du mig som en Løve, handlede atter ufatteligt med mig;
17 Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
nye Vidner førte du mod mig, øged din Uvilje mod mig, opbød atter en Hær imod mig!
18 “Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
Hvi drog du mig da af Moders Liv? Jeg burde have udaandet, uset af alle;
19 Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
jeg burde have været som aldrig født, været ført til Graven fra Moders Skød.
20 Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
Er ej mine Livsdage faa? Saa slip mig, at jeg kan kvæges lidt,
21 kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
før jeg for evigt gaar bort til Mørkets og Mulmets Land,
22 nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”
Landet med bælgmørkt Mulm, med Mørke og uden Orden, hvor Lyset selv er som Mørket.

< Ayubu 10 >