< Ayubu 1 >

1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
There was a man in the land of Uz named Job, and he was a simple and honest man, fearing God and withdrawing from evil.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
And there had been born to him seven sons and three daughters.
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
And his possession was seven thousand sheep, and three thousand camels, along with five hundred pairs of oxen and five hundred she-donkeys, and also a very large family. And this man was great among all the people of the east.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
And his sons went and made a feast by houses, each one on his day. And sending, they called their three sisters to eat and drink with them.
5 Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
And when the days of their feasting had been completed, Job sent to them and sanctified them, and, getting up at dawn, he offered holocausts for each one. For he said, “Perhaps my sons have sinned and have not praised God in their hearts.” So Job did all the days.
6 Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
But on a certain day, when the sons of God came to attend in the presence of the Lord, Satan also arrived among them.
7 Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
The Lord said to him, “Where do you come from?” Answering, he said, “I have circled the land, and walked around in it.”
8 Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
And the Lord said to him, “Have you not considered my servant, Job? For there is no one like him in the land, a simple and honest man, fearing God and withdrawing from evil.”
9 Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
Answering him, Satan said, “Does Job fear God to no purpose?
10 Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
Have you not fortified him, as well as his house and every one of his belongings around him, blessed the works of his hands, and his possession has increased in the land?
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
But extend your hand a little, and touch all that he possesses, and see if he still praises you to your face.”
12 Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
Therefore, the Lord said to Satan, “Behold, everything that he has is in your hand, only do not extend your hand against him.” And Satan departed from the face of the Lord.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
So, on a certain day, when his sons and daughters were eating and drinking wine, in the house of their first-born brother,
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
a messenger came to Job, who said, “The oxen were plowing, and the donkeys were grazing beside them,
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
and the Sabeans rushed in and carried away everything, and they struck the servants with the sword; and I alone evaded them to tell you.”
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
And while he was still speaking, another arrived, and he said, “The fire of God fell from heaven, and, having struck the sheep and the servants, it consumed them; and I alone escaped to tell you.”
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
And while he also was still speaking, another arrived, and he said, “The Chaldeans organized three attacks, and advanced on the camels and took them; and not only that, but they have struck the servants with the sword; and I alone fled to tell you.”
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
He was still speaking, and behold, another entered, and he said, “Your sons and daughters were feasting and drinking wine in the house of their first-born brother,
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
when suddenly a severe wind rushed forth from a region of the desert and shook the four corners of the house, which collapsed and crushed your children, and they are dead; and I alone escaped to tell you.”
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
Then Job got up and tore his garments, and, having shaved his head, he collapsed on the ground, and worshipped,
21 na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
and he said, “Naked I departed from my mother’s womb, and naked I shall return. The Lord gave, and the Lord has taken away. Just as it pleased the Lord, so has it been done. Blessed be the name of the Lord.”
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
In all this, Job did not sin by his lips, nor did he speak any foolish thing against God.

< Ayubu 1 >