< Ayubu 1 >

1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Uz ram dawk tami buet touh ao teh, a min teh Job doeh. Ahni teh toun hane awm hoeh, tamikalan, Cathut ka taket e, kahawihoehe lamthung ka roun e lah ao.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
Capa 7 touh hoi canu 3 touh a tawn.
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
A tawn e naw teh, tu 7,000, kalauk 3,000, maitotan 500, lamanu 500, hoi a sannaw moikapap a tawn. Ahni teh Kanîtholae taminaw pueng hlak tami ka lentoe poung e lah ao.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
A capanaw ni kum tangkuem amamae a khenae pawi a sak awh navah, amamae im dawk bu canae pawi a sak awh teh a kamkhueng awh navah, a tawncanunaw ka 3, touh hai canei hanelah ouk a coun.
5 Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
Hottelah bu canae pawi abaw hnukkhu vah, Job ni a kaw awh teh, ouk a kamkhueng sak awh. Amom a thaw teh ahnimae milu kuep lah hmaisawi thuengnae sathei ouk a poe. Bangkongtetpawiteh Job ni ka capanaw ni yonnae sak awh vaiteh, a lungthin hoi Cathut hah pahnawt awh langvaih telah ati. Hottelah, Job ni pou a sak.
6 Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
Cathut e capanaw BAWIPA e hmalah tâconae hnin a pha torei teh, Setan hai ahnimouh koe a tho van.
7 Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
BAWIPA ni Setan koe nâ lahoi maw na tho atipouh. Setan ni BAWIPA talai van ka kâhei teh ka kumluennae koehoi, atipouh.
8 Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
BAWIPA ni Setan koe ka san Job he na pouk boimaw. Talai van dawk ahni patetlae toun han kaawm hoeh e, tamikalan Cathut ka taket e hoi, kahawihoehe lamthung ka roun e awm hoeh, telah atipouh.
9 Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
Setan ni BAWIPA a pathungnae teh, Job ni Cathut hah a khuekhaw awm laipalah maw a taki.
10 Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
Ahni teh a imthung hoi, a tawn e naw pueng hoi, a tengpam pueng pet na kalup teh, a kut hoi a tawk e naw pueng hah yawhawi na poe teh, na kamphung sak nahoehmaw.
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
Atuvah na kut pho nateh a tawn e hnonaw pueng hah tek pouh haw, na hmaitung roeroe vah nama tang na pahnawt han doeh atipouh.
12 Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
BAWIPA ni, Setan koe, khenhaw! a tawn e naw pueng teh, nange na kut dawk ao. Ama teh tek hanh atipouh. Hahoi Setan teh BAWIPA koehoi a tâco.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
Hnin touh hnin teh, a canu hoi a capanaw teh, a hmau kacue im dawkvah a ca awh teh misurtui a nei awh lahun nah,
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
Job koe patoune buet touh a yawng teh, maitotannaw talai a kanawk awh lahun nah, lanaw hai ateng a pâ awh lahun navah,
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Sheba taminaw ni na tuk awh teh, koung a la awh toe na sannaw hah tahloi hoi a thei awh teh, kai buet touh dueng doeh, nang koe dei hanelah ka hlout atipouh.
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
A dei lahun nah tami alouke bout a tho. Kalvan hoi Cathut e hmai a bo teh, tu hoi na sannaw hah koung a kak teh be a kahma toe. Kai buet touh dueng doeh nang koe dei hanelah ka hlout e lah ka o atipouh.
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
A dei lahun nah tami alouke bout a tho. Khaldean taminaw ahu kathum touh lah ao awh teh, kalauknaw hah koung na lawp awh, na sannaw hai tahloi hoi be a thei awh. Kai buet touh dueng doeh nang koe dei hanelah ka hlout atipouh.
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
A dei lahun nah tami alouke bout a tho. Na canu hoi na capanaw ni, a hmau kacuepoung e im vah a ca awh teh misurtui a nei awh lahun navah,
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
Khenhaw! kahrawng lahoi kahlî katang poung e a tho teh, imnaw hah a hmang teh, thoundoun, tanglanaw hah koung a ratet teh koung a due. Kai buet touh dueng doeh nang koe dei hanelah ka hlout atipouh.
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
Hahoi Job ni a thaw teh, ahni a ravei, a lû luengpalueng lah a ngaw teh, talai dawk a tabo teh a bawk.
21 na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
Anu e von thung hoi tak caici lah ka tâco teh, tak caici lah bout ka ban han. BAWIPA ni na poe teh BAWIPA ni bout a la. BAWIPA min teh pholennae awm seh telah a ti.
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
Hetnaw dawkvah Job ni yonnae sak laipalah Cathut yonpennae tawn hoeh.

< Ayubu 1 >