< Yeremia 9 >
1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Qui donnera à ma tête de l’eau, et à mes yeux une fontaine de larmes? et je pleurerai jour et nuit les morts de la fille de mon peuple.
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Qui me donnera dans la solitude une cabane de voyageur, et j’abandonnerai ce peuple, et je me retirerai d’eux? parce que tous sont adultères, troupe de prévaricateurs.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
Et ils ont tendu leur langue comme un arc de mensonge et non de vérité: ils se sont fortifiés sur la terre, parce qu’ils ont passé d’un mal à un autre mal, et ils ne m’ont pas connu, dit le Seigneur.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
Que chacun se garde de son prochain, et qu’il ne se fie à aucun de ses frères; parce que tout frère supplantant supplantera son frère, et que l’ami marchera frauduleusement.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
Et chaque homme se rira de son frère, et ils ne diront pas la vérité; car ils ont formé leurs langues à parler mensonge; ils ont travaillé à iniquement agir.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Ta demeure est au milieu de la tromperie; c’est par tromperie qu’ils ont refusé de me connaître, dit le Seigneur.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
À cause de cela voici ce que dit le Seigneur des armées: Voilà que je les fonderai, et que je les éprouverai par le feu: car que ferai-je autre chose vis-à-vis de la fille de mon peuple?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
C’est une flèche blessante que leur langue; elle a parlé tromperie; chacun en sa bouche parle paix avec son ami, et en cachette il lui tend des pièges.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Est-ce que je ne visiterai pas ces crimes, dit le Seigneur, ou d’une pareille nation mon âme ne se vengera-t-elle pas?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
Sur les montagnes je m’abandonnerai aux larmes et aux lamentations; et sur les belles contrées du désert, aux plaintes, parce qu’elles ont été brûlées, pour qu’il n’y ait pas d’homme qui y passe; on n’a pas entendu la voix du possesseur; depuis l’oiseau du ciel jusqu’aux troupeaux, tous ont émigré et se sont retirés.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
Et je ferai de Jérusalem des monceaux de sable et un repaire de dragons; et les cités de Juda, je les livrerai à la désolation, pour qu’il n’y ait point d’habitant.
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Quel est l’homme sage qui comprenne ceci, et à qui la parole de Dieu soit adressée, afin qu’il l’annonce, qui comprenne pourquoi cette terre a péri, qu’elle a été brûlée comme un désert, pour qu’il n’y ait pas d’homme qui y passe?
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
Et le Seigneur a dit: C’est parce qu’ils ont abandonné ma loi que je leur ai donnée, et qu’ils n’ont pas écoute ma voix, et qu’ils n’ont pas marché en elle;
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
Et parce qu’ils ont suivi la dépravation de leur cœur, et les Baalim; ce qu’ils ont appris de leurs pères.
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
C’est pourquoi, voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Voilà que je nourrirai ce peuple d’absinthe, et je lui donnerai pour breuvage de l’eau de fiel.
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
Et je les disperserai parmi des nations qu’ils n’ont point connues, eux et leurs pères, et j’enverrai après eux le glaive, jusqu’à ce qu’ils soient consumés.
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Regardez attentivement, et appelez les pleureuses, et qu’elles viennent; envoyez à celles qui sont sages, et qu’elles s’empressent;
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
Qu’elles se hâtent, et qu’elles fassent entendre sur nous des lamentations; que nos yeux versent des larmes, et que de nos paupières coulent des eaux.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
Parce qu’une voix de lamentation a été entendue de Sion: Comment avons-nous été ravagés et couverts d’une grande confusion? puisque nous avons abandonné notre terre, et que nos tabernacles ont été abattus.
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Ecoutez donc, femmes, la parole du Seigneur; que vos oreilles saisissent le discours de sa bouche; enseignez à vos filles les lamentations, et que chacune apprenne à sa voisine les cris plaintifs;
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
Parce que la mort est montée par nos fenêtres, qu’elle est entrée dans nos maisons, pour exterminer les petits enfants au dehors, et les jeunes hommes dans les places publiques.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Parle: Voici ce que dit le Seigneur: Et le cadavre de l’homme tombera comme le fumier sur la face de la terre, et comme l’herbe derrière le dos du moissonneur, et il n’y a personne qui la recueille.
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Voici ce que dit le Seigneur: Que le sage ne se glorifie point dans sa sagesse; que le fort ne se glorifie point dans sa force, et que le riche ne se glorifie point dans ses richesses;
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
Mais que celui qui se glorifie se glorifie de cela, de me connaître, et de savoir que c’est moi qui suis le Seigneur, qui fais miséricorde et jugement, et justice sur la terre; c’est là ce qui me plaît, dit le Seigneur.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
Voici que les jours viennent, dit le Seigneur, et que je visiterai quiconque est circoncis,
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
L’Egypte, Juda, Edom, les fils d’Ammon et de Moab, ceux dont la chevelure est coupée, qui habitent dans le désert; parce que toutes ces nations sont incirconcises de corps, et toute la maison d’Israël est incirconcise de cœur.