< Yeremia 9 >

1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Qui donnera à ma tête un réservoir d'eau, et à mes yeux une source de larmes? Et je pleurerai mon peuple nuit et jour, et la mort de la fille de mon peuple.
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Qui me donnera, dans le désert, une cabane lointaine? Et j'abandonnerai mon peuple, et je m'éloignerai de lui; car ce sont tous des adultères, c'est une assemblée de prévaricateurs.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
Et ils ont tendu leur langue comme un arc; le mensonge, et non la bonne foi, a prévalu sur la terre; car ils ont passé de péché en péché, et ils ne m'ont point connu.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
Gardez-vous chacun de votre prochain, ne vous fiez pas à votre frère: tout frère supplantera son frère; tout ami s'approchera traîtreusement de son ami.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
Chacun se joue de ses amis; on ne dit pas la vérité. Leur langue a appris à dire des mensonges; ils ont commis l'injustice; ils ne font rien pour se convertir.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Usure sur usure, fraude sur fraude; ils n'ont point voulu me connaître.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Je les ferai passer par le feu, et je les éprouverai, et j'agirai ainsi en voyant la perversité de la fille de mon peuple.
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
Leur langue est une flèche acérée; les paroles de leur bouche sont trompeuses; au prochain, on parle de paix, et on a la haine au cœur.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Est-ce que je ne les visiterai pas pour ces choses? dit le Seigneur; est- ce que mon âme ne tirera pas vengeance d'un tel peuple?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
Faites entendre une lamentation sur les montagnes, chantez un cantique funèbre dans les sentiers du désert; car ces lieux sont désolés faute d'hommes. On n'y entend plus la voix d'êtres vivants, depuis les oiseaux du ciel jusqu'aux troupeaux: ils ont été frappés de stupeur, et ils ont fui.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
Et je ferai sortir de Jérusalem ses habitants, et elle sera la demeure des dragons; et je mettrai la désolation dans les villes de Juda au point qu'elles ne seront plus habitées.
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Quel homme est assez intelligent pour comprendre ces choses? Et la parole du Seigneur viendra à lui; qu'il vous annonce pourquoi la terre a péri, et a été brûlée comme un désert, au point qu'on n'y peut plus passer.
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
Et le Seigneur me dit: C'est parce qu'ils ont abandonné la loi que je leur ai donnée face à face, et n'ont pas écouté ma voix.
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
Mais ils ont couru après les convoitises de leur cœur pervers, et après des idoles que leurs pères leur avaient appris à adorer.
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
A cause de cela, dit le Seigneur Dieu d'Israël, voilà que je vais les nourrir d'angoisses et les abreuver d'eau mêlée de fiel.
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
Et je les disperserai parmi les nations, chez des hommes que ni eux ni leurs pères n'ont connus; et je ferai tomber sur eux le glaive, jusqu'à ce que le glaive les ait détruits.
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Voici ce que dit le Seigneur: Appelez des pleureuses, et qu'elles viennent; envoyez chercher les plus habiles à pleurer, et qu'elles élèvent la voix.
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
Et qu'elles chantent une lamentation sur vous, et que des larmes tombent de vos yeux, et que vos paupières soient inondées de pleurs.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
Car leur voix lamentable a été entendue en Sion: Comment sommes-nous réduits à cet état de misère, tellement confondus que nous avons abandonné notre terre et renversé nos tabernacles?
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Femmes, écoutez la parole de Dieu, et que vos oreilles recueillent les paroles de sa bouche: Apprenez à vos filles des lamentations, apprenez-vous les unes aux autres des cantiques funèbres:
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
Parce que la mort est montée par vos fenêtres, et qu'elle est entrée dans vôtre terre pour exterminer au dehors les enfants à la mamelle, et dans les rues les adolescents.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Et les cadavres des hommes resteront en exemple sur la surface de votre terre, comme le chaume reste derrière le moissonneur; et nul ne sera là pour les recueillir.
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Voici ce que dit le Seigneur: Que le sage ne se glorifie pas dans sa sagesse; que le fort ne se glorifie pas dans sa force; que le riche ne se glorifie pas dans sa richesse.
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
Mais que celui qui se glorifie se glorifie de comprendre et de savoir que c'est moi le Seigneur, moi qui fais sur la terre miséricorde, jugement et justice; car c'est en cela que je me complais, dit le Seigneur.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
Voilà que les jours viennent, dit le Seigneur, où je visiterai tous les circoncis en leur chair,
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
Et l'Égypte, et l'Idumée, et Édom, et les fils d'Ammon, et les fils de Moab et tous ceux qui se coupent la chevelure au-dessus du front, et qui habitent le désert; car tous ces peuples sont incirconcis en leur chair, et toute la maison d'Israël incirconcise en son cœur.

< Yeremia 9 >