< Yeremia 9 >

1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Oh! ma tête, que n’est-elle des eaux, et mes yeux, une fontaine de larmes! et je pleurerais jour et nuit les blessés à mort de la fille de mon peuple!
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Oh! qui me donnera dans le désert une cabane de voyageur! et j’abandonnerais mon peuple et je m’en irais d’avec eux; car ils sont tous des adultères, une assemblée de perfides.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
Et ils bandent leur langue, leur arc de mensonge, et ils ne sont pas vaillants dans le pays pour la fidélité; car ils passent d’iniquité en iniquité, et ne me connaissent pas, dit l’Éternel.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
Gardez-vous chacun de son ami, et ne vous confiez en aucun frère; car tout frère ne fera que supplanter, et tout ami marche dans la calomnie.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
Et chacun d’eux trompe son ami, et ne dit pas la vérité; ils ont enseigné leur langue à dire le mensonge, ils se fatiguent à faire le mal.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Ton habitation est au milieu de la tromperie; à cause de la tromperie ils refusent de me connaître, dit l’Éternel.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
C’est pourquoi, ainsi dit l’Éternel des armées: Voici, je vais les affiner et les éprouver; car comment agirais-je à l’égard de la fille de mon peuple?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
Leur langue est une flèche mortelle, elle profère la tromperie; de sa bouche il parle de paix avec son ami, mais au-dedans il lui dresse des embûches.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Ne les punirais-je pas à cause de ces choses? dit l’Éternel; mon âme ne se vengerait-elle pas d’une nation comme celle-là?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
J’élèverai une voix de pleurs et une lamentation sur les montagnes, et une complainte sur les pâturages du désert, car ils sont brûlés, de sorte que personne n’y passe et qu’on n’y entend pas la voix des troupeaux; tant les oiseaux des cieux que les bêtes ont fui; ils s’en sont allés.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
Et je ferai de Jérusalem des monceaux [de ruines], un repaire de chacals; et des villes de Juda, j’en ferai une désolation, de sorte qu’il n’y aura plus d’habitant.
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Qui est l’homme sage? qu’il comprenne cela. Et celui à qui la bouche de l’Éternel a parlé, qu’il le déclare! Pourquoi le pays périt-il, [et] est-il brûlé comme un désert, de sorte que personne n’y passe?
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
Et l’Éternel dit: Parce qu’ils ont abandonné ma loi que j’avais mise devant eux, et qu’ils n’ont pas écouté ma voix, et parce qu’ils n’ont pas marché en elle,
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
et qu’ils ont marché suivant le penchant obstiné de leur cœur et après les Baals, ce que leurs pères leur ont enseigné.
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
C’est pourquoi, ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Voici, je vais faire manger de l’absinthe à ce peuple, et je leur ferai boire de l’eau de fiel;
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
et je les disperserai parmi les nations qu’ils n’ont pas connues, eux et leurs pères; et j’enverrai après eux l’épée, jusqu’à ce que je les aie consumés.
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Ainsi dit l’Éternel des armées: Considérez, et appelez les pleureuses, et qu’elles viennent; et envoyez vers les femmes sages, et qu’elles viennent,
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
et qu’elles se hâtent, et qu’elles élèvent une [voix de] lamentation sur nous, et que nos yeux se fondent en larmes, et que l’eau coule de nos paupières.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
Car une voix de lamentation se fait entendre de Sion: Comme nous sommes détruits, [et] devenus fort honteux! car nous avons abandonné le pays, car ils ont jeté à bas nos demeures.
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Vous, femmes, écoutez donc la parole de l’Éternel, et que votre oreille reçoive la parole de sa bouche; et enseignez à vos filles la lamentation, et chacune à son amie la complainte.
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
Car la mort est montée par nos fenêtres, elle est entrée dans nos palais, pour retrancher de la rue les petits enfants, [et] des places, les jeunes hommes.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Dis: Ainsi dit l’Éternel: Oui, le cadavre de l’homme tombera comme du fumier sur la face des champs, et comme la gerbe après le moissonneur, et il n’y a personne qui la recueille.
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Ainsi dit l’Éternel: Que le sage ne se glorifie pas dans sa sagesse, et que l’homme vaillant ne se glorifie pas dans sa vaillance; que le riche ne se glorifie pas dans sa richesse;
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
mais que celui qui se glorifie, se glorifie en ceci, qu’il a de l’intelligence et qu’il me connaît; car je suis l’Éternel, qui use de bonté, de jugement et de justice sur la terre, car je trouve mes délices en ces choses-là, dit l’Éternel.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
Voici, des jours viennent, dit l’Éternel, et je punirai tous les circoncis avec les incirconcis,
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
l’Égypte, et Juda, et Édom, et les fils d’Ammon, et Moab, et tous ceux qui coupent les coins [de leur barbe], lesquels habitent le désert; car toutes les nations sont incirconcises, et toute la maison d’Israël est incirconcise de cœur.

< Yeremia 9 >